Riwaya - Mtoto Tamu Nyotika - Utamu / VIta / Fantansia

 

Mama kwa haraka akaniziba mdomo wangu huku tukiwa tumejibanza kwenye migomba mingi sana, iliyopo karibu kwenye kijumba chetu cha udongo huku tukimshuhudia baba akipigwa kipigo na watu walio valia mavazi meusi huku wakiwa wamezificha sura zao kwa vitambaa. Bariki kali na mvua kubwa inayo endelea kunyesha katika eneo hili la kijiji chetu cha Umbwe hapa Moshi, ikamfanya mama azidi kunikumbatia huku akilia kwa sauti ya chini chini sana. Machozi na hasira zikazidi kunitawala, ila sina uwezo wa kufanya kitu chochote nikiwa bado ni mtoto mdogo mwenye umri wa miaka sita.

“Wewe si unajifanya mjanja kuwashawishi wakulima wezako kukataa mimi kuwekeza kwenye hichi kijiji si ndio?”

Sauti ya mwanaume aliye zungukwa na watu hawa wanao endelea kumtesa baba ilisikika vizuri, japo mama alijitahidi kuniziba macho yangu nisishuhudie kitendo hicho anacho fanyiwa baba yangu, ila nikazidi kujitahidi kuangalia ila mama aliigeuza sura yangu pembeni na nikaendelea kunikumbatia. Niliendelea kusikia miguno ya baba yangu na kilio chake cha maumivu.

“Sasa utakufa kama shujaa mpuuzi, mpigeni hadi afe na mwili wake mukautupe shambani kwake”

Sauti ya mwaunaume huyo iliyoa maagizo hayo na kuwafanya watu hao kuendelea kumpiga baba kwa magongo mazito. Kwa bahati mbaya ikapiga radi mwanga wake ukaangaza kila eneo hili.

“Kuna watu kule kwenye migomba”

Kijana mmoja alizungumza huku akinyoosha mkono wake kwenye eneo hili tulilo jificha na mama. Kwa haraka mama akanishika mkono wangu wa kuli na hapakuwa na budi tena zaidi ya kuanza kukimbia.

“Lole kimbia”

Mama alizungumza huku akiniachia mkono na kuanza kuchechemea.

“Ndefo mama”(Mama twende)

Nilizungumza kwa lugha ya kichaga huku nikijaribu kumshika mkono mama ila mama kwa ishara akaniomba nikimbie kwani watu hao wanazidi kutukaribia. Machozi ya yakazidi kunimwagika usoni mwangu, kwani sina uwezo wa kupambana na wanaume hawa na wala sina uwezo wa kumtetea mama yangu. Mama kwa ishara ya mkono akazidi kunisisitizia niweze kukimbia ili kuyaokoa maisha yangu.

Nikakimbia kwenye hii migomba mingi, huku nyuma nikaanza kusikia sauti ya mama yangu akipiga mayowe ya kuomba msaada. Ila mvua na mingurumo hii ya radi na umbali tulipo kutoka jirani mmoja hadi mwengine ni swala ambalo ni gumu sana kusikika. Kila nilipo jaribu kusonga mbele, nikajikuta nikisita kabisa kuendelea na safari hii. Nikaangaza angaza chini na kuona fimbo, nikaichukua na kuanza kurudi eneo nilipo muacha mama yangu huku machozi yakinimwagika usoni mwangu na hasira ikiwa imejaa kifuani mwangu.

Nikafika katika eneo ambalo yupo mama yangu, nikawakuta vijana hawa sita wakimbaka kwa nguvu, jambo lillo nifanya nianza kumchapa mmoja wao.

“Ametokea wapi huyo mtoto”

Kijana mmoja ambaye ndio yupo katikati ya mapaja ya mama alizungumza huku akiwa amevua kitambaa kilicho kuwa kimeiziba sura yake.

“Mpigeni”

“Mkuu ila huyu ni mtoto”

“Mtoto mpigeni na mumuue”

“Ja….ma…..ni….musi….mp……”

Mama alizungumza kwa shida sana kwani amepigwa kipigo kizito sana na kubwa juu.

“Muondoeni hapa”

Kijana huyo anaye endelea kumuingilia mama kinguvu alizungumza na vijana wake wawili wakanishika na kunibebe juu juu. Nikajitahidi kwa nguvu zangu zote ili mradi niweze kujitoa mikononi mwao na kwenda kumsaidia mama ila utoto wangu na kuto kuwa na nguvu, ukawafanya vijana hawa kunihimili. Vijana hawa wakaendelea kunibeba huku wakinitandika magofi mazito pamoja na ngumi katika kila sehemu ya mwili wangu.

“Tumuue”

Kijana mmoja alizungumza kwa ukali huku wakinibwaga chini kama mzigo wa kuni.

“Hapana huyu ni mtoto mdogo sana, hatuna haja ya kumuua”

“Tumepewa agizo na mkuu?”

“Ni bora tumtupe huko kwenye korongo, akafie mtoni”

Niliweza kuyasikia mazungumzo ya vijana hawa vizuri sana, ila uwezo wa kusimama sina kwa maana wamenipiga sana ngumi na makofi kana kwamba wana mpiga mtu mzima mwenzao. Wakanisukumia bondeni kwenye korongo kubwa na nikaanza kumbingirika huku nikipia kelele za kuomba msaada, ila galfa nikahisi kishindo kikubwa kichwani mwangu na taratibu macho yangu yakapoteza uwezo wa kuona na sikujua ni nini kinacho endelea.

***

Nikaanza kusikia sauti ya watu wawili wakizungumza huku mmoja akiwa ni mwanamke. Sauti ninazisikia ila kile wanacho kizungumza kwangu ndio mtihadi kabisa kwani ni lugha ambayo siifahamu. Nikafumbua macho yangua, taratibu ila ukungua mwingi ulio yatawala macho yangu ukanifanya nisiweze kuona watu hao.

“Heii boy”

Niliisikia sauti ya kike ikizungumza pembeni yangu.

“Ameamka”

“Unajisikiaje kijana?”

Watu hawa waliendelea kuniuliza maswali ambayo sikuweza kuyajibu kwa maana siwaoni vizuri.

“Unaweza kuzungumza?”

Mwanamke aliniuliza kwa sauti ya upole.

“Tumuache apumzike kwa muda ndio tumulize maswali”

“Ila ni kijana mzuri sana”

“Yaa sijui ni kwa nini waswahili wanawanyanyasa watoto hivi”

Nikajaribu kumtazama mwanaume huyu, taratibu nikaanza kuiona sura yake, ni mzee wa kizungu mwenye mvi nyingi sana kichwani mwake. Nikamtazama mwanamke aliye simama pembeni ya mzee huyu, naye ni bibi wa kizungu, ila hajazeeka sana kama huyu mzee.

“Mtengenezee supu nzuri ya kuku”

Mzee huyu alizungumza, bibi huyo akambusu mumewe shavuni kisha wakatoka ndani hapa. Mzee huyu akavuta stuli na kukaa pembeni ya hichi kitanda. Akaanza kunishika shika mguu wangu wa kushoto, taratibu nikautazama mguu wangu na kujiona nikiwa nimefungwa bandeji kwenye mguu mzima. Nikaanza kulia, kwa maumivu niliyo anza kuyahisi mara tu ya kuuona mguu wangu.

“Hapana kijana usilie”

“Nipo wapi…...?”

Niliendelea kulia huku nikijitahidi kukaa kitandanii. Mzee huyu akajitahidi na kunirudisha na kulala. Maumivu ya kichwa nayo yakazidi kunichanganya. Mzee huyu akachukua moja ya bomba la sindano lenye dawa na kunichoma mkononi mwangu. Taratibu nikaanza kuhisi usingizi ulio nifanya nilale fofofo ndani ya muda mchache tu.

***

Baada ya siku mbili nikapata nafuu kidogo hata ya kuka mwenyewe kitandani, mzee Klopp na mke wake Bi Jane Klopp, kama walivyo jitambuisha jana, wakaniomba waweze kuzungumza na mimi. Kwa haraka haraka katika kipindi hichi cha siku hizi mbili nilizo kaa nao wamekuwa ni watu wa kunijali kwa kila jambo. Muda wao mwingi wanautumia katika kunitazama na kujua hali yangu inaendeleaje.

“Unaitwa nani?”

Bi Jane Klopp aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Eheee?”

“Unaitwa nani?”

Nikajaribu kukumbuka jina langu, ila nikajikuta nikishindwa kulikumbuka kabisa.

“Je unajua ni nini kimekukuta?”

Bi Jane Klopp aliendelea kuniuliza kwa upole, ila nikashindwa kabisa kufahamu ni kitu gania mbacho kimenipata.

“Hapana, kwani nipo wapi?”

Niliuliza kwa suati ya upole na unyonge.

“Upo Arusha mjini”

“Nimefikaje fikaje?”

Bibi Jane Klop wakatazamana na mume wake huku wakionekana kujawa na mshangao sana.

“Okay, siku chache zilizo pita tulikuwa Moshi, kwenye matembezi yetu ya kufanya uchunguzi ulio tuleta huku nchini Tanzania, kwa bahati nzuri tuliweza kukuta kwenye moja ya mto ukiwa umepoteza fahamu, ilikuwa ni alfajiri sana.”

Mzee Klop alizungumza kwa upole huku akinitazama usoni mwangu.

“Tulipo kuchunguza vizuri tukagundua kwamba upo hai, tukaona sio mbaya tukakusaidia kwa maana bado ni mtoto mdogo sana”

“Asanteni”

“Usijali, ni jukumu letu. Je unakumbuka kama una ndugu, au marafiki ambao tunaweza kuwasiliana nao wakaja kukuchukua hapa?”

Nikatingisha kichwa huku nikijitahidi kuvuta japo taswira ya mtu yoyote ninaye mfahamu kwenye maisha yangu ila sikuweza kukumbuka. Kitu kilichopo hapa kichwani mwangu ni hawa wazee wawili mbele yangu.

“Kutokana hapa Tanzania tumebakisha muda mchache wa kukaa, basi tutafanya mpango wa kuondoka na wewe na kurudi nchini Ujerumani yalipo makazi yetu sawa”

“Sawa”

“Na kuanzia leo utaitwa Ethan Klopp, hilo ndio litakuwa ni jina lako”

“Ethan Klopp?”

“Ndio hilo ndio jina lako kuanzi hii leo”

Nikatabasamu kidogo kwani ni jina zuri kwa upande wangu na wala sioni sababu ya kukataa kulikataa kwa maana jina langu halisi silifahamu.

“Na sisi tutakuwa ni wazazi wako, kwa maana tuna binti yetu mmoja tu yupo nchini Ujerumani, na wewe utakuwa ni mtoto wetu wa pili sasa”

“Ninashukuru sana”

Nikajikuta furaha ikinitawala moyoni mwangu. Taratibu bibi Jane Klopp akanikumbatia kwa nguvu, huku akitawaliwa na furaha.

Siku zikazidi kusonga mbele huku hali yangu ikizidi kuimarika, matibabu anayo nipatia bibi Jane Klopp na mume wake yananifanya nizidi kuwa imara. Wakaanza kunifundisha vitu vingi, na wakazidi kushangazwa na uwezo wangu wa akili kwani katika kipindi cha muda mchache kila wanacho nifundisha basi ninakielewa kwa haraka na ni vigumu sana kuweza kukisahau. Wakaanza kunifundisha Kijerumani, japo ni lugha ngumu kidogo ila nikajitahidi hivyo hivyo ndani ya mwezi mzima nikawa tayari nipo vizuri kwenye lugha hiyo na hawa wakiniongelesha ninaweza kuwaelewa na kuwajibu kiufasaha.

“Ethan unajua wewe ni genius?”

Bibi Jane Ethan aliniambia tukiwa jikoni nikimsaidia kuandaa chakula cha usiku.

“Genius ndio nini?”

“Ni mtu mwenye upeo mkubwa wa kiakili, tofauti na watu wengine”

“Mtu akiwa hivyo ndio anaitwa Genius?”

“Ndio, ninakuahidi, nitahakikisha kwamba tunakupatia elimu bora unakuwa mtu bora kabisa hapa duniani”

“Nashukuru sana mama”

Bibi Ethan kama kawaida yake akainama kidogo na kunibusu kwenye paji langu la uso ikiwa ni ishara ya upendo ambao amenizoesha kuanzia siku ya kwanza kuanza kuishi nao.

“Ukiwa mkubwa Ethan unapenda kuwa nani?”

“Mmmmmm……nahitaji kuwa na nguvu?”

“Hahaaa…..hata hapo mbona una nguvu. Au unataka kuwa na nguvu ya kisiasa, kiuchumi au ushawishi katika jamii?”

“Yoyote tu ila nahitaji kuwa na nguvu tu”

“Hupendi kuwa dokta, au rubani?”

“Mmmmmmhhhh”

“Kweli?”

“Ndio mama”

“Basi kama nitaendelea kupewa maisha marefu basi nitahakikisha kwamba unakuwa na nguvu mwanangu”

“Nashukuru sana mama”

Tukaendelea kuandaa chakula hichi cha usiku, hatukuchukua muda mrefu sana tukafanikiwa kumaliza kupika, nikasaidana na bibi Klopp kutenga chakula mezani, baada ya maandalizi hayo yote kunalizika nikaelekea chumbani kumuita baba ambaye ni mzee Klopp.

“Ohooo nina kuja sasa hivi?”

“Sawa baba”

Nikaanza kuelekea mlangoni, ila kabla sijafika mlangoni akaniita, nikageuka na kumtazama, kwa ishara ya mkono akaniita na nikafika hadi kwenye kiti alicho kaa huku akiwa ana andika andika vitu kwenye kipakato chake(laptop)

“Kuna shule za primary, nilikuwa ninazitafuta hapa, nahitaji tukirudi Ujerumani uende ukasome, je ni ipi kati ya hizi mbili ni ipi hapa unaipenda?”

Mzee Klop alinonyesha majengo makubwa mawili ya shule zilizopo kwenye nchi ya Ujerumani ambapo kila siku nina tamani siku zao za kuishi hapa nchini Tanzania ziishe ili nirudi nao Ujerumani.

“Hii hapa”

Nilizungumza huku nikimuonyesha jengo moja zuri.

“Umeipenda hii?”

“Ndio baba”

“Sawa, tena hizi ni shule za watoto wenye uelewa maalumu. Tumeweza kugundua kwamba una uwezo huo”

“Nashukuru baba”

Unyenyekevu na utii ndio ngao yangu kubwa sana ya kuendelea kuishi na wazee hawa, malengo yangu na nia yangu ni kuhakisha kwamba nina pata nguvu kubwa kwenye maisha yangu, na nilazima yatime pale tu nitakapo kuwa mtu mzima. Tukatoka kwa pamoja humu chumbani na kurudi sebleni, tukapata chakula cha usiku kwa pamoja kisha tukasali ibada ya usiku kama ilivyo kuwa desturi waliyo jiwekea. Baada ya sala wao wakaelekea chumbani kwao na mimi nikaelekea chumbani kwangu na kulala.

Baada ya siku wiki tatu, kuisha, siku ya kuondoka nchi Tanzania ikawadia, kila hatua zote za kiserikali za kuondoka na mimi nchini humu walizikamilisha, japo sifahamu sana kuhusiana na mambo hayo. Tukapanda ndege ya shirika la Fast Jet hadi jijini Dar es Saalam ikiwa ndio mara yangu ya kwanza kufika katika jiji hili ambalo nilikuwa nikilisikia sikia tu kipindi cha nyuma kwamba ndio jiji zuri sana hapa nchini Tanzania.

‘Lazima nitawale hili jiji siku’

Nilijikuta nikila kiapo moyoni mwangu huku nikitazama magorofa marefu, tukiwa njiani tunaelekea katika hoteli ya karibu ili kupumzika kwa muda ili kesho asubuhi na mapema tuweze kuondoka na ndege kuelekea nchini Ujerumani. Tukafika hotelini, mzee Klopp na mkewe wakachukua chumba kimoja, huku na mimi wakinipangishia chumba changu. Baada ya kupata chakula cha usiku, tukaelelea katika vyumba vyetu ili kupumzika ili kesho alfajiri na mapema tuwe tumewasili katika uwanja wa ndege. Shauku na hamu ya kwanza ya kupanda ndege, nimesha imaliza kwa kupanda ndege kutoka Moshi hadi jijini hapa Dar es Salaam. Shauku yangu ya pili ni kwenda nchini Ujerumani kuishi kabisa. Uzuri wa mataa katika magorofa mengi ninayo yaona kwa mbali, ukanifanya muda wangu mwingi sana niutumie nikiwa nimesimama dirishani hapa nikishangaa taa hizi.

‘Nilazima uwe na nguvu ya kuawala hili jiji’

Niliisikia sauti nzito akilini mwangu iliyo nistua kidogo na kunipa wasiwasi. Damu mwili mzima ikaanza kunisisimka na vinyweleo vyangu vikaanza kusimama. Mapazia yaliyopo pembeni yangu hapa dirishani yakaanza kupepea, jambo lililo zidi kunifanya niwe na wasiwasi kwa maana madirisha ni ya vioo na yote yamefungwa vizuri sana na hakuna nafasi ya upepo kuweza kuingia na kuyafanya mapazia haya kutikisika.

‘Ethan…..Ethan…….Ethan……’

Niliisikia sauti ya kiume ikiniita kwa mbali, nikajaribu kuangaza macho yangu ndani ya chumba hichi ili niweze kuona ni nani anaye niita ndani ya hichi chumba ila sikuweza kuona zaidi ya mapazia kuendelea kutingishika sana. Woga ukanijaa, mwili mzima ukazidi kunitetemeka.

“ETHAN……..”

Sauti hii nzito nikaisikia vizuri kwenye masikio yangu, taa zote ndani ya chumba hichi zikazima na nikaona kivuli cha mtu chenye mwanga hafifu sana kikiwa kimesimama kwenye moja ya ukuta wa humu chumbani huku kivuli hicho kikionesha mtu huyo akiwa amevaa joho kubwa sana, ila haonekani kichwa ni kipi wala miguu ni ipi jambo lilo nifanya niaguke chini mzima mzima huku nikitamani kupiga kelele ila sauti yangu haikuweza kutoka.

 

 

“Usiogope, mimi sio mbaya kwako”

Sauti ya mwanaume huyu ikazidi kuniongelesha, jasho lililo tokana na joto kali likazidi kuniandama.

“Najua nini unacho kiwaza na kukifikiria. Nitakusaidia, kadri siku zitakavyo zidi kwenda ndivyo kadri nitakavyo zidi kuwa rafiki yako na msaada wako kwako. Usimuambie mtu wa aina yoyote habari hii umenielewa?”

Nikamjibu kwa kutingisha kichwa nikimaanisha kwamba nimelewa.

“Endapo utazungumza chochote kwa mtu yoyote basi mtu huyo nitamuua. Lala salama na usiku mwema”

Mara baada ya mwanaume huyo kuzungumza hivyo, taa zote zikawaka na kila kitu kikarudi kwenye hali yake, hapakuwa na pazia hata moja ambalo liliweza kutingishika. NIkasimama kwa haraka na kuanza kutembea hadi mlangoni ili nikawaeleze Bi Jane Klopp na mumewe habari hizi, ila nilipo kumbuka kwamba endapo nitamualeza yoyote atakufa, basi hamasa hiyo ya kuwaambia, ikaanza kutetea na mwishowe nikajikuta nikirudi kitandani mwangu na kuaa. Kusema kweli katika siku ambazo sikuwahi kulala ni hii ya leo, sauti ya mwanaume huyu ambaye sifahamu ni nani ikazendelea kujirudia kwenye masikio yangu.

Nikastuka baada ya kengele iliyo fungwa mlangoni humu kuanza kuita, nikatazama saa ya ukutani nikaona ni majira ya saa kumi na moja kasoro alfajiri. Nikakumbuaka kwamba jana usiku bibi Jane Klopp aliniahidi kwamba atakuja kuniamsha muda huu ili nianze kuajiandaa kwa ajili ya safari kwa maana ndege yetu inaondoka saa kumi na mbili asubuhi. Kengele ikaendelea kuminywa, taratibu nikashuka kiyandani na kuanza kutembea hadi mlangoni, nikaufunga mlango nakweli nikamkuta bibi Jane Klopp akiwa amejawa na tabasamu pana sana usoni mwake.

“Umeamkaje Ethan?”

“Salama mama, wewe je?”

Niliitikia huku nikijifanya kama nina usingizi mwingi, ila kwa namna moja ama nyingine sina usingizi wa aina yoyote zaidi ya woga wa tukioa ambalo nilikutano nalo jana usiku.

“Tumeamka salama, jiandae tuianze safari”

“Sawa mama”

“Haya”

Bi Jane Klopp akaondoka mlangoni kwangu, nikafunga mlango na moja kwa moja nikalifwata sehemu begi langu la nguo lilipo, nikafungua zipo ya pembeni, nikatoa mswaki wangu pamoja na dawa yake, kisha nikaelekea bafuni. Nikasafisha kinywa changu, ndani ya muda mfupi nikiwa tayari nimesha maliza kukisafisha kinywa hichi. Nikaoga haraka haraka kisha nikarudi chumbani, nikavaa nguo nilizo kusudia kuzivaa katika safari hii, ambayo tayari hamu yake imerudi kwenye mstari hata tukio lililo tokea jana usiku likaanza kunipotea kwenye upeo wangu wa akili.

Nilipo hakikisha kwamba nimemaliza kila kitu, nikamuomba Mungu kama nilivyo fundishwa na Bi Jane Klopp, ili awe kunitangulia katika safari hii, kisha nilipo maliza sala yangu, nikatoka chumbani humu huku nikilivuta begi langu. Kwa bahati nzuri nikakutana na Bi Jane Klopp pamoja na mzee Klopp wakitoka kwenye chumba chao huku nao wakiwa tayari wamesha jianda. Nikamsalimia mzee Klopp kwa heshima zote, kisha tukaelekea nje ya hoteli hii na kumkuta yule dereva ambaye alituleta jana hapa hotelini akiwa tayari amesha fika kama vile alivyo elezwa na bi Jane Klopp aweze kuwahi asubuhi na mapema kwenye hotel hii.

Baada ya dereva kuingiza mabegi yetu nyuma ya taksi yake hii, mimi na bi Jane Klop tukaingia kwenye siti ya nyuma huku Mzee Klopp akipanda siti na kukaa siti ya mbele pamoja na dereva.

“Ethan mwanangu, unajisikiaje?”

Bi Jane Klopp aliniuliza huku akiwa amenishika mkono wangu wa kulia huku akiminya minya kiganja changu.

“Ndio mama, nina furaha sana”

“Unakwenda kuyaanza maisha mapya sasa Ethan”

“Kweli baba ninakwenda kuanza maisha mapya”

“Ila tutakuwa tunarudi Tanzania mara kadhaa, kuitembele hii nchi si unafahamu kwamba hii ndio nchi yako”

“Ndio mama”

“Hata ikatokea kwamba tumekufa, ila Tambua uhalisia wako wewe ni upi, wapi umetoka na tunaamini kwamba ipo siku utakutana tena na ndugu zako”

“Sawa mama”

Swala la ndugu zangu bado kwa upande wangu ni kitendawili, nina jaribu kuvuta kumbukumbu za kumkumbuka japo hata mama yangu wa kunizaa ila sipati hata taswira yake. Tukafika uwanja wa ndege, tukapitia hatua zote ambazo kama abiria anatakiwa kupitia, muda wa abiria kuelekea kwenye ndege tunayo paswa kusafiri nayo, ukawadia. Tukaingia kwenye ndege hiyo bibi Jane Klopp na mumewe wakaa katika siti za mbili huku mim nikikaa siti ya pembeni yao, ila na abiria mwengine ambaye ni mwana mama wa kiafrika. Nikamsalimia mwana mama huyu kwa heshima sana, hadi mwenyewe akanishangaa. Akaitikia salamu yangu huku akiwaametabasamu.

“Unaitwa nani mtoto?”

“Ethan Klopp”

“Anaa mimi naitwa mama Lukas”

“Nashukuru kukufahamu mama Lukas”

“Unasafiri peke yako?”

“Hapana, nipo na wazazi wangu, hao hapo”

Nikawaonyesha Bi Jane Klopp na mume, ambao nao kwa furaha wakasalimiana na mama huyu.

“Kusema kweli nimetokea kukupenda sana mtoto…..  nyota ya mtoto inaanza kung’aa kabla hajafika ujerumani… nini kitatokea … matamanio makubwa anayopitia …

Riwaya hii ina visa vizito vya kimapenzi, vita, matukio ya mshangao….

 

Whatsapp - +255 758 018 597

KURASA ZAIDI YA 500 KWA 1000 TU

 

 


Post a Comment

0 Comments