“We binti njoo hapa,”
nilikuwa napita kwenye mtaa mmoja kule Temeke, nikaitwa hivyo na mbaba mmoja
aliyekaa kwenye benchi la kijana anayeosha viatu, wenyewe mnamuita
‘shuushaina’!
Kwa jinsi yule mbaba
alivyonitumbulia macho, mwenyewe nikaogopa, nikajikuta nimemfuata…
“Shikamoo,” nilimwamkia
huku nikiangalia pembeni kwa woga.
Mimi nilitarajia
ataniambia amenifananisha na msichana anayemjua…
“Marhaba! Unaitwa nani
wewe?”
“Rhoda.”
“Rhoda nani?” aliniuliza
kwa ukali mpaka nikataka kukimbia. Moyoni nikasema ‘he! Huyu mbaba vipi? Mbona
ana maswali kama polisi wa Kilwa Road?’
“Rhoda Musalanga,”
nilimjibu.
“Unakaa wapi?”
“Kule juu Wailesi.”
“Kwa mzee nani?”
“Khaa! Kwa mzee nani
kivipi? Si kwa baba yangu!” nilijipa ujasiri na kumjibu hivyo…
“Baba yako anaitwa nani?”
kabla sijamjibu, nilimwona yule kijana msafisha viatu akiachia tabasamu.
Niliamini amejua swali la yule mbaba ni la kijinga…
“Jamani, si nimekwambia
naitwa Rhoda Musalanga, si ndiyo baba yangu mzazi…”
“Una simu?” aliniuliza
swali jingine. Ina maana swali lake la awali alishalijua jibu lake.
“Kwani we unataka nini?”
“Nataka nini! Si nataka
namba yako ya simu, hebu nitajie,” aliniambia huku akiwa amenitumbulia macho.
Sijui ilikuaje, si nikajikuta nikizitoa namba zangu. Nilimtajia moja baada ya
nyingine, kisha akatumbukiza mkono mfukoni na kutoa noti mbili za shilingi elfu
kumi…
“Hizi utakunywa
soda…umeolewa?”
“Akha! Mi sijaolewa,”
nilimjibu kwa kukataa mpaka na mabega.
Kifupi mimi nilikuwa
nimemaliza masomo ya sekondari na nina miaka 22 tu, lakini kutokana na umbo
langu kuwa kubwa, wengi waliamini niko kwenye ndoa tayari.
Kwanza nilikuwa mrefu, si
mnene sana lakini pia si mwembamba. Umbo langu ni namba nane! Katikati katikati
kweli, juu kifuani palijaa sawasawa na katikati kwenda chini nilijengeka kama
vile nilitengenezwa kwenye kiwanda cha magari cha Mjapan.
“Nitakuoa mimi… we
nenda,” aliniambia yule mbaba huku akimwangalia msafisha viatu.
Kwangu lilikuwa tukio la
ajabu sana. nilifika nyumbani na kukaa kimya, sikumwambia mama wala dada yangu,
Agatha. Najua ningemwambia dada Agatha angeniambia nimpeleke na yeye kwa yule
mbaba.
Nilikwenda Temeke kwenye
maduka makubwa, nikanunua makufuli yangu matano kwa zile pesa, nikazidi kuwa wa
kisasa zaidi. Maana mtaani naitwa Amber Rose kutokana na umbo langu lilivyo. Na
vijana wengi walishatangaza dau mpaka la pesa nyingi ili wanipate lakini
walikosa bahati hiyo, akaipata mmoja tu, Mwafyale ambaye ana duka la vipodozi
Temeke Mwisho.
Sasa niliishi nikitegemea
kupata ujumbe wowote kutoka kwa yule mbaba maana mimi sikuwa na namba yake.
Kweli bwana, saa saba juu
ya alama mchana akanipigia simu, nikapokea haraka sana maana nilikuwa na shauku
ya kutaka kujua nia yake kwangu…
“Hujambo?”
“Sijambo…shikamoo…”
“Unaamkia mara ngapi kwa
siku?”
“Nilisahau, samahani
sana…”
“Utakula jeuri yako…uko
wapi?”
Nilitamani kwanza kujua
maana ya mimi kula jeuri yangu kabla hata ya kumjibu nilipo. Lakini nikahisi ni
msemo, nikamjibu swali lake…
“Mimi niko nyumbani…”
“Wapi?”
“Si nilikwambia
jamani…huku mitaa ya Wailesi…”
“Utakula jeuri yako…njoo
hapa mitaa ya Temeke Hospitali…mimi nakaa hapa,” alisema kwa sauti ya ukali
iliyojaa amri…
“Kwani huyu mbaba ni
nani? Mbona amri amri…mtu simjui hanijui halafu ananiamuru kama mwanaye, kwa
nini lakini?” niliwaza moyoni, lakini nikashindwa kumuuliza…
“Nije kufanya nini
sasa..?”
“We…utakula jeuri
yako…unajifanya hujui siyo?”
“Mimi sijui!”
“Wewe njoo utajua kwa
nini nimekuita.”
“Mkeo je?”
“Sina…”
“Mh! Wewe ulipo hapo huna
mke kweli?”
“Nilimfukuza.”
“Kwa nini?”
“Haikuhusu…wewe njoo
haraka.”
Nilijikuta nikimpa dakika
kumi na tano tu kwamba, nitakuwa nimefika mitaa hiyo.
Niliingia bafuni kuoga
chapuchapu kisha nikavaa. Tena kwa ndani nilivaa kufuli moja mpya. Nje
nikapigilia suruali ya skin’taiti nyeusi na blauzi juu nyeupe, miguuni sendoz,
nikaondoka zangu bila kumuaga mama wala dada.
Nilipofika mitaa ya
hospitali nilimtwangia simu, haraka sana akapokea…
“Oya mi nipo hapa
hospitali…”
“Njoo moja kwa moja mpaka
kwenye kontena mbele hapa, utanikuta.”
Nilitembea kunyoosha njia
mpaka kwenye kontena, nikamkuta amekaa na wenzake wawili wakinywa bia. Yeye
alivaa pensi na fulana…
“Kaa hapa…wee mletee bia
huyu yoyote lakini ya baridi,” alimwambia mhudumu.
Niseme ukweli, nakunywa
pombe kwa hiyo agizo hilo kwangu halikuwa geni na aliyenifundisha kunywa pombe
ni jamaa yangu, Mwafyale, mwenyewe nimezoea kumwita Mwana FA.
“Yoyote?” aliuliza
mhudumu. Mhudumu mwenyewe ni jianajike f’lani. Ukimwangalia hivi ana sura ya
kufumaniwafumaniwa tu…
“Kwani huuzi bia?” yule
mbaba aliuliza…
“Sasa si nimekwambia lete
yoyote lakini ya baridi…”
“Eti anti, nikupe bia gani?”
“Yoyote.”
Yule mhudumu aliondoka
akicheka.
Baada ya kunywa bia moja,
mbaba alinisimamisha na kuniambia…
“Twende huku la sivyo
utakula jeuri yako.”
Jamani wewe…wapi sasa?”
“Hutaki?”
“Siyo kama sitaki…nataka
kujua tunakwenda wapi?”
“Si kule…mimi si mtu
mbaya kwako. Ningekuwa mbaya ningekupa pesa yangu? Twende.”
Maneno yake yalikuwa kama
kumsukuma mlevi, kwani nilijikuta miguu ikikubali kwenda yenyewe bila
kulazimishwa huku nikiwa najishangaa.
Tulikwenda kuingia kwenye
nyumba moja kubwa sana. Ina vyumba huku na huku, katikati ni korido pana.
Ilionekana kila chumba kilijitegemea. Kwa hiyo hakukuwa na chumba na sebule.
Ilikuwa maalum kwa ajili ya kupanga tu.
Basi, yule mbaba aliingia
kwenye chumba cha katikati kwa kufungua kufuli na funguo alizokuwa nazo.
“Karibu, pita,”
aliniambia huku akinipitisha mlangoni, akaweka pazia la mlango vizuri kisha
akaufunga kwa kitasa cha ndani…. Whatsapp kupata full +255 758 018 597 au pakua Kulaya Simulizi App kupitia hii link
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.swahili.simulizi&hl=en
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.swahili.simulizi&hl=en
0 Comments
Karibu sana, tuma ujumbe whatsapp +255 758 018 597 kujipatia simulizi zetu
Emoji