Bebi,
bado natafuta mbona utaenjoy sana tu nakupenda toa mawazo yako hayo,
"Nalijua hilo lakini mi nina wivu juu yako, na hata kazi yako sijaipenda
huyo mwanamke anaekurudisha kila siku kwa gari na kwanini umuambie mimi dada
yako, yaani naumia sana mume wangu wa kunifanyia hivi kweli kila kitu
umesahau""Kwani nini kinachoharibika? mimi nafanya hivi ili tuwe na
maisha mazuri, nimeshakuambia niamini hutaki aaa mi nawahi kibaruani
bwana" aliongea kijana huyo aliefahamika kwa jina la Saidi na kumuacha
mpenzi wake akiwa na sitofahamu kichwani mwake. Mrembo huyo aliefahamika kwa
jina Maimuna alijiinua kiunyonge akufurahia hata penzi lake kwa Saidi, Saidi
nae akumpa huduma zinazostahiki kama mkewe. Umri wake unajitosheleza kuwa na
watu wenye pesa lakini alibaki kwa Saidi wake, na Saidi aliishi na Maimuna
baada ya kumpa mimba, tena walikuwa kidato cha 4, Maimuna shule aliacha hata
Saidi aliacha nae na penzi lao liliwashangaza wengi ndipo wazazi wa mamuna
waipokuja juu mno ikamlazimu Maimuna ampeleke Saidi nyumbani kwao. Na Saidi
yeye alikuwa hana wazazi hivyo alikuwa akiishi na uncle wake, wazazi wa Maimuna
walimwangalia ninyi yao na kumtazama Saidi wakaona wote ni watoto na wameamua
kuishi wawili basi wazazi walipitisha swala hilo tena awakumtoza Saidi hata
senti wazazi walitaka aishi na binti yao vizuri ndipo Saidi amebeba majukumu
mazito, aliangaikia kibarua akapata. Alipiga kazi huku akiakikisha Maimuna
anaishi vizuri na hasa mwanae alie tumboni. Siku zilisogea wawili hao wakiishi
pamoja ndipo siku moja mkewe alizidiwa na kwakuwa Saidi pesa zilikuepo akiba
ndipo akaaamua kukodi taxi na kumpeleka hospitali, alisubili majibu lakini
daktari majibu aliyompa yalifanya asikitike. Mkewe Maimuna amejifungua lakini
mtoto kafariki Saidi alitamani aitwe baba akiwa na miaka 21 tu lakini haikuwa
hivyo, na tangu tukio hilo Saidi upendo ulipungua kwa mkewe na akaja kupata
kazi ya shamba boy kwenye Nyumba ya kitajiri, nyumba hiyo ilikuwa ya familia ya
watu wanne yaani baba, mama, kijana wao wa kiume na binti yao wa kike. Saidi
alipewa jukumu la kumchunga binti huyo aliefahamika kwa jina Natasha. Ilifika
wakati Natasha alimzoea Saidi na akawa anampeleka kwa gari mpaka nyumbani
kabisaa na kitu hicho kilimkera sana Maimuna, alijua tu anaibiwa penzi lake
lakini Saidi ni Wa kujitetea siku zote, Saidi alimuacha mkewe akilalama na
kuondoka zake kazini, alifika na kuingia ndani na kumkuta Natasha yuko bize na
mambo yake. Natasha alipotupa macho alimuona Saidi aliacha mambo yake na
kumkimbilia, alipomfikia alimkumbatia"vipi Saidi
wangu""poa" alijibu jibu la mkato na kutoa mikono ya Natasha
kiunoni kwake"acha bwana Natasha utaniaharibia kazi mi si
nipo""mi sitaki bwana, mi nataka uje kukaa hapa kwetu we uwoni aibu
kukaa na dada yako nyumba moja""hayo achana nayo yule sister wangu
hivyo yaani""Ok sasa mbona anaonyesha ana wivu juu yako utafikiri mtu
wake kumbe! mh""achana nae ni sister wangu tu" aliongea hayo
Saidi akionyesha dhahiri usaliti kwa mkewe, muda ulishaenda Natasha alitoa
kiasi cha pesa na kumkabidhi, kisha akamsindikiza tena kwa gari. Natasha
alimpeleka Saidi kwake, walipofika huko Saidi alishuka kwenye gari na kumsihi
Natasha asishuke lakini Natasha hakuwa muelewa Saidi aliingia ndani na kumkuta
Maimuna kajilaza zake sakafuni, Saidi alimstua mkewe kwa kumpiga miguuni"oh
mume wangu huyo vp huko""Safi tu mbona umelala
unaumwa""Hapana nimechoka tu mume wangu, basi ngoja nikuandalie
chakula mume wangu""Mh mi sio mlaji kiukweli nisikuongopee mke wangu
mi nishakula huko nilipotoka si unajua kazi yangu hii""Mimi nimepika
chakula kingi lakini mwenzangu umeshiba? lakini mbona umebadilika
laazizi""Mke wangu wivu wako umepitiliza sasa too much sasa, mimi
siku hizi nitakuwa nikilala huko huko maana aaa""Sasa kazi gani hiyo
unajua fika kuwa mimi ni mkeo lakini hujali hilo, huonyeshi mapenzi yoyote sawa
tu""aa ushaanza yani sina raha nawe kwanza kuna mgeni wangu nahitaji
nimsindikize maana nimemueka kweli nje" aliongea hayo Saidi na punde tu
Natasha aliingia ndani na kumshika Saidi mkono"Umeshasahau kama umeniacha
nje.. Whatsapp +255 758 018 597.
Hakikisha umefollow Page yetu Mpya ya Instagram kwa kubofya Link hapa chini.Tunahitaji wewe ndio uffolow kwakuwa ni member wa swahilisimulizi.com
Hakikisha umefollow Page yetu Mpya ya Instagram kwa kubofya Link hapa chini.Tunahitaji wewe ndio uffolow kwakuwa ni member wa swahilisimulizi.com
https://www.instagram.com/swahilisimulizi/ Full story
whatsapp +255 758 018 597
0 Comments
Karibu sana, tuma ujumbe whatsapp +255 758 018 597 kujipatia simulizi zetu
Emoji