Haikuwa rahisi kuamini kuwa moja ya kitu alichokifuata Gosbert
katika chuo kikuu kilicho makao makuu ya nchi na serikali na chuo kinachobeba
jina la mkoa maarufu unaosifika kwa uzalishaji wa zao litengezalo divai na
mvinyo, ilikuwa kusomea digrii ya kwanza ya taaluma ya elimu na nyongeza ya
digrii ya pili katika uhusiano na mapenzi. Hakika Gosbert aliwika kama jogoo
aliyekuwa katika kipindi cha kubarehe kwa kuwasumbua kina dada katika chuo
hicho. Hakuna sketi iliyokatisha mbele yake ikiwa na ubora asitake kujua ndani
ilibeba kitu gani. Hata katika makundi ya mijadala ya masomo ya usiku watu
walimwogopa kwa kazi yake ya urijali wa jogoo kuwika na kupanda mtungi. Hakika
kwa tabia aliyoionyesha hapo chuoni wanachuo wenzake walimpachika jina la Dokta
Love almaarufu kama Mr. Lover boy. Jina hilo lilisadifu uhalisia wa tabia yake
kwani aliwafunua sketi mabinti wadogo hata wanawake walio umri sawa na mama
yake. Hakika Gosbert alisifika kama shujaa maalum aliyemfano wa jogoo kwa
kuwika katika vifua vya wanawake. Gosbert alikuwa amekwishaharibu katika block
B namba 98 kwa kuonja utamu wa kila binti na mwanamke aliyekuwemo ndani chumba
hicho. Tabia ya kuwika na kusimama juu ya vifua vya kina dada iliwakera na
kuamua kumshikisha adabu kijana huyo wa bush aliyeuvamia mji kwa staili ya
pekee ya kuutafuta utamu wa mapenzi na ladha ya kupendwa katika moyo wake.
Christina aliinua simu yake na kubonyeza namba fulani kisha akaweka sikioni na
kuanza kusikia simu ikiita upande wa pili na kupokelewa,
"Haloo
bebi wangu mambo vipi!Nimekumisije baba?Njoo basi room jamani"
"Uko
block gani na chumba namba ngapi"
"Niko
block B chumba namba 98. Njoo mpenzi wangu jamani. Uniletee na chipsi mayai
sawa baba!"
"Hilo
wala usijali mama!Nitakuwa hapo baada ya dakika kama ishirini hivi. Uko na kina
nani. ?"
"Niko
mwenyewe baby, wenzangu wametoka, wamekwenda town kula bata na wapenzi wao.
Njoo ufaidi penzi tamu baba. . .
"Sawa
mama nitakuja muda si mrefu, nitegemee baada ya sekunde kadhaa, nitakuwa hapo.
"
Simu ilikatwa
na kuwekwa mezani huku vicheko vikitawala katika chumba hicho. Kama wasemavyo
waswahili kipya hakinyemi ingawa kidonda tena upya wa. . . . . . . . . . .
Gosbert aliiona nafasi hiyo adimu kwake kama golden chance ya kufaidi penzi
jipya toka kwa first year na hakutaka kuipoteza kwa siku hiyo. Masikini Gosbert
kama angelijua mtego ulio mbele yake asingethubutu kuinua miguu yake na
kuelekea katika block aliloelekezwa. Mtego ulioandaliwa ulikuwa na lengo
la kumnasa paka anayedokoa mboga jikoni na kumbabua kwa moto mkali. Dakika chache
na sekunde kadhaa baadae Gosbert alionekana akikwea ngazi kuelekea floor ya nne
chumba namba 98. Gosbert alikuwa akitupa macho juu ya namba za milango
iliyokuwa katika floor hiyo. Mara macho yake yalitua katika mlango ulioandikwa
namba 98. Aliusogelea mlango huo kisha akaugonga ngo!ngoo!
"Hodi
humu ndani!Hodi wenyewe!"
Gosbert
alinyonga kitasa hicho ili kimruhusu aingie ndani lakini kitasa hicho
kilimkodolea macho na kumwambia asubiri ruhusa kutoka ndani kwa wenyeji wake.
Christina aliwaambia wenzake wajifiche ili wamnase mwizi wao anayechezea na
kudhalilisha miili yao. Christina aliuendea mlango akaingiza funguo na kunyonga
kitasa kilichouruhusu mlango kufunguka na kulakiwa na tabasamu la mgeni wake.
Gosbert aliingia ndani huku akielekezwa aketi katika deka ya chini ya kitanda
kilicho kushoto pembeni ya mlango. Christina alifunga vizuri mlango na kuuondoa
ufunguo katika kitasa kisha alirejea kitandani na kuketi karibu na Gosbert.
Gosbert alimkabidhi mfuko mweusi uliohifadhi viazi ulaya vilivyoshikamana na
mayai pamoja na vipande vya nyama vilivyotungwa kwa ustadi katika vijiti
maalum. Christina uliupokea mfuko ule na kuuweka mezani, kisha akamuuliza
Gosbert,
"Samahani
baby, mbona hujaniletea soda jamani. "
"Tazama
vizuri mpenzi, soda imo ndani ya huo mfuko. "
Gosbert
hakupoteza muda, alimsogelea Christina na kuanza kumkumbatia huku
akimpiga mabusu ya nguvu shavuni mwake. Katika hali ya kustaajabisha Gosbert
alihisi……
0 Comments
Karibu sana, tuma ujumbe whatsapp +255 758 018 597 kujipatia simulizi zetu
Emoji