“Prosper!
Prosper! Prosper! Mshike baba yako ataniua!” Alisema mama huyo na baadaye kukaa
kimya huku akiendelea kutoka damu, hiyo ndiyo ilikuwa kawaida mama huyo aliishi
kwa mateso jambo lililomkera sana Prosper na dada zake.
“Baba
mwache mama! Kwanini unampiga hivyo si keshakufungulia mlango?”
“Wee
unanishika unataka kunichangia na mama yako siyo?”
“Sitaki
kukupiga baba lakini naomba usimpige mama kiasi hicho hana kosa!”
Wakati
Prosper akiongea maneno hayo tayari Kasanda na Nyamizi walishafika na
kumnyanyua mama yao aliyekuwa amelala chini akiwa amepoteza fahamu huku damu
nyingi zikimtoka mdomoni, midomo yake ya juu na chini ilikuwa imevimba kwa
ngumi aliyopigwa na mume wake, wakambeba na kumpeleka chumbani kwao ambako
walimmwagia maji akarejewa na fahamu.
“Mama
twende polisi!” Kasanda alimshauri mama yake.
“Hapana
watoto wangu tukienda polisi baba yenu atafungwa! isitoshe sisi Wanyamwezi
hatutakiwi kabisa kushtaki polisi tunapopigwa na waume zetu”
Watu
wote katika kijiji cha Tutuo barabara ya kwenda Sikonge walikoishi Prosper na
wazazi wake walitambua ukorofi wa mzee Kabaka na hakuna mtu aliyediriki
kumkemea, kila mtu alimuogopa.
Kama
ungefanikiwa kukutana na mama Kalunde, sio siri machozi yangekutoka, alikuwa ni
mama wa makamo, mrefu mwenye umbile la kitutsi,rangi ya ngozi yake ilikuwa
nyeusi lakini iliyojaa makovu mengi, kwa kumwangalia ungegundua kabisa kuwa
mama huyo aliwahi kuwa tishio wakati wa ujana wake!
Alikuwa
ni mama mwenye mateso, alipigwa karibu kila siku na mume wake,hakuwa na sikio
moja tayari lilishakatwa na mumewe! Jicho lake la kulia lilikuwa chongo baada
ya kupasuliwa na mume wake wakati wa kupigwa miaka miwili kabla ya siku hiyo!
Alikuwa ni mama aliyepata mateso makubwa mno katika maisha yake ya ndoa.
Wakati
hayo yote yakitokea Prosper alikuwa na umri wa miaka 17 akimalizia kidato cha nne
katika shule ya sekondari ya Sikonge, pamoja na matatizo aliyokuwa nayo
alifanikiwa kuchaguliwa kuendelea na kidato cha tano katika shule ya sekondari
ya St.Magreth ilikuwa ni shule ya bweni, na ilikuwa ni lazima aende kuishi
bwenini akiwaacha dada zake Kasanda na Nyamizi pamoja na wazazi wake.
“Prosper
tutaweza kweli kumhimili baba akimpiga mama?”
“Mungu
atawasaidia dada zangu sina budi kwenda shule ili niwasaidie baadaye!” Prosper
aliwaeleza dada zake wakati wa kuagana, akaondoka kwenda zake Moshi shuleni.
Alipofika
shuleni kwa mara ya kwanza alikuwa amechelewa na kilichomchelewesha zaidi
ilikuwa ni ada, mama yake Kalunde alilazimika kufanya vibarua katika mashamba
ya watu ili aweze kupata pesa za kumwezesha Prosper kwenda shule! Baba yake
hakujali kabisa.
“Prosper
mwanangu usifanye michezo shuleni, si unaona maisha yetu yalivyo na unaona
nilivyohangaika? Baba yako hana msaada wowote, yeye ni pombe kila siku na
kunipiga mimi tu, familia nzima tunakutegemea wewe uje kuwa mkombozi wetu
kajitahidi mwanangu!”
“Sitakuangusha
mama nakuahidi! “
“Sawa
mwanangu!”
Darasa
lao lilikuwa na wafunzi hamsini na mbili kati yao wasichana wakiwa kumi na
saba! Ni Prosper peke yake aliyeonekana kuwa na uwezo mdogo kifedha na watu
wengi walimdharau, alikuwa na nguo zilizochanika na madaftari yake yalikuwa ni
ya kurasa shirini na nne ambayo hayakutumiwa na wanafunzi wengi shuleni hapo!
Yalidaiwa kuwa ya watoto wa shule za msingi.
Pamoja
na umasikini wake Prosper alijitahidi sana na masomo kama alivyomuahidi mama
yake na hiyo ni kwa sababu aliifahamu familia yake, alitaka asome ili apate
uwezo wa kuwakomboa ndugu zake, barua zilizokuja kutoka nyumbani kwao
zilimweleza juu ya kipigo alichopata mama yake na Prosper alilia.
Wanafunzi
wengi walimtenga sababu ya umasikini wake isipokuwa msichana mmoja tu aliyeitwa
Belinda!Msichana huyo alimsaidia Prosper kwa vitu vingi shuleni ikiwemo Sabuni,
mafuta na hata sukari na wakatokea kuwa marafiki wakubwa.
Katika
mtihani wa mwisho wa muhula aliwashangaza wengi pale alipoibuka na kushika
namba ya kwanza kati ya wafunzi wote! Ni matokeo hayo ndiyo yalianza kumpa
heshima na marafiki wengi shuleni.
Shule
zilipofungwa kwa sababu Prosper hakuwa na nauli ya kumrudisha hadi nyumbani
kwao Tabora, ilibidi abaki shuleni peke yake akijisomea! Alimkumbuka sana mama
yake na alitaka kwenda nyumbani lakini kwa sababu hakuwa na nauli alilazimika
kubaki peke yake shule nzima.
Shule
zilipofunguliwa wanafunzi wote walirejea shuleni na yeye na Belinda msichana
aliyeonekana kutoka familia tajiri jijini Dar es Salaam, walisoma na kufanya
kila kitu pamoja Belinda alikuwa miongoni mwa wasichana wagumu kuelewa masomo
yao, lakini Prosper alitumia muda wake mwingi kumfundisha hatimaye akawa
miongoni mwa wasichana waliofanya vizuri katika mitihani yao.
Mwisho
wa muhula wa pili Prosper alishika tena namba ya kwanza darasani kwake na
Belinda aliibuka katika kumi bora! Kila mtu mpaka walimu wake walishangaa,hilo
liliukomaza zaidi uhusiano wao.
“Prosper
utakwenda Tabora likizo hii?”
“Mimi?
Mimi? Hapana sitakwenda!”
“Kwanini?”
“Sina
nauli ya kunipeleka nyumbani nendeni tu mtanikuta!”
“Hapana
Prosper this time ni lazima uende!”
“Nitakwenda
na nini sina nauli Belinda?”
“Nitakupa
nauli ya kukupeleka na kukurudisha!” Alisema Belinda.
Prosper
hakuamini aligeuka na kumwangalia Belinda usoni, wote wawili walijikuta
wakitabasamu na baadaye kukumbatiana na kuanza kupigana mabusu usoni, Belinda
alijaribu kuupenyeza ulimi wake kuuingiza mdomoni kwa Prosper lakini Prosper
aliuma meno yake kuonyesha hakupenda kitu hicho kitokee!
“Belinda
unataka kufanya nini?”
“Nakupenda
Prosper tafadhali tunyonyane ndimi!”
“Nitatapika
Belinda sijawahi kufanya kitu kama hicho hata siku moja!”
Belinda
alishindwa kuendelea lakini alijua ni kwanini Prosper alisema hivyo, alimwachia
na wakaendelea na safari yao kuelekea mabwenini kujipumzisha wakisubiri siku
inayofuata.
Asubuhi
kitu cha kwanza alichofanya Belinda ni kumkabidhi Prosper kiasi cha shilingi
80,000 kwa ajili ya nauli ya kumpeleka Tabora na kumrudisha shuleni.
“Belinda
mbona pesa hizi ni nyingi sana!”
“Zitakazobaki
utawanunulia wazazi na ndugu zako zawadi!”
“Ahsante
Belinda, sikutegemea!”
“Ahsante
wewe kwani bila wewe mimi nisingefanikiwa kimasomo? Isitoshe nakupenda Prosper huwezi
kupata taabu wakati mimi nina kitu!”
“Belinda
mzazi wako ni nani hasa hapa nchini?” Ilibidi Prosper aulize, sababu
alishangazwa na msichana mdogo kama Belinda kuwa na kiasi kile chapesa.
Belinda
alimweleza kila kitu kilichokuwepo katika maisha yake, alieleza pia juu ya
utajiri wa baba yake na jinsi baba yake alivyompenda sababu alikuwa mtoto pekee
wa kike! Hakuacha kumweleza juu ya mama yake wa kambo.
“Nina
kila kitu nyumbani isipokuwa upendo wa mama, mama yangu wa kambo ananitesa
sana, hanipendi amewafanya hata kaka zangu wa kambo pia wanichukie!”
“Unafikiri
ni kwanini?”
“Kwa
sababu wanajua baba ananipenda na kuna uwezekano wa kupata sehemu kubwa sana ya
mali yake akifa, hiyo nafikiri ndiyo sababu kubwa!”
“Pole!”
“Ahsante,
lakini nataka uelewe nakupenda na tukirudi kutoka likizo safari hii nataka kila
mtu aelewe jambo hapa shuleni ili wavulana waache kunisumbua!”
“Huogopi
kuchekwa Belinda!”
“Kwanini?”
“Sababu
mimi ni masikini!”
“Nakupenda
kwa jinsi ulivyo Prosper!”
Ni
kweli Prosper alikuwa na sura ya kumvutia kila mwanamke kilichomsumbua kilikuwa
ni umasikini.
Prosper
alikata tiketi ya treni na kusafiri hadi Tabora mjini ambako alipanda mabasi ya
kumpeleka hadi nyumbani kwao Tutuo, kiasi cha kilometa sabini hivi kutoka
Tabora mjini, njia nzima alimfikiria mama yake alitaka sana kumwona!
Ulikuwa
umepita muda mrefu bila kuonane naye! Mawazo juu ya dada zake na baba yake
hayakumuumiza kichwa sana, alimuwazia mama yake zaidi, alimpenda sana na
hapakuwa na mtu mwingine kama mama maishani kwake!
Aliposhushwa
na basi kituoni kitu cha kwanza alichofanya ni kukimbia dukani na kununua
vitenge doti tatu kwa ajili ya mama yake na pia alinunua magauni mawili kwa
ajili ya dada zake, Nyamizi na Kasanda! Hakusahau kumnunulia baba yake suruali
nzuri! Moyo wake ulijaa furaha, alikuwa na hamu kubwa mno ya kuiona familia
yake tena.
Baada
ya manunuzi hayo alinyoosha moja kwa moja kwenda nyumbani kwao,njiani akiwa
amebeba begi lake alishangaa jinsi ambavyo watu walimwangalia na kuonyesha
masikitiko.
Alipofika
nyumbani kwao hakuna mtu aliyejitokeza kumpokea, mlango wa nyumba ulikuwa wazi,
ilibidi aingie hadi ndani akiliita jina la mama yake, lakini hakuitikiwa,
mwisho alianza kuita majina la dada zake lakini bado ilikuwa kimya.
Wakati
bado akijiuliza maswali kichwani mwake alitokea rafiki yake mkubwa aliyeitwa
Kategile na kusimama mbele yake.
“Pole
sana Prosper bahati mbaya umechelewa mazishi!”
“Ya
nani?” Aliuliza kwa mshangao Prosper.
“Baba
yako!”
“Baba?”
“Ndiyo!”
“Baba
kafariki lini?”
“Wiki
iliyopita!”
Prosper
alianza kulia na majirani wengine zaidi walifika na kuanza kumpa pole,
walishangaa kuwa hakuwa na taarifa hizo!”
“Sasa
mama na ndugu zangu wapo wapi?”
“Wapo
kituo cha polisi kati mjini Tabora”
“Wamefanya
nini?”
“Ni
wao ndio walimpiga baba yako na kumuua!”
Siku
iliyofuata asubuhi Prosper alikwenda moja kwa moja kituo cha polisi kati
kuwaona ndugu zake pamoja na mama yake, alilia machozi alipomwona mama yake
akiwa mahabusu, aliomba kuongea naye akaruhusiwa na wakapewa chumba yeye na
mama yake pamoja na dada zake waongee.
“Mama
kweli mlimuua baba?”
“Mwanangu
nililazimika kufanya hivyo kwani alichukua kisu na kunikata sikio langu la
pili…..”Mama yake Prosper alianza kulia.
“Alilitoa?”
“Halipo
mwanangu, nimepoteza masikini yangu yote mawili baba yako alikuwa katili mno
alistahili kufa na ninakiri nimemuua!”
“Ulimuua
na nini?”
“Nilimpiga
na mchi kichwani akaanguka na kufa! Huo ndio ukweli mwanangu!”
“Mama
ulishindwa kweli kufuata ushauri wangu?”
“Nisamehe
mwanangu!”
“Mama
hautafia gerezani ni heri nifungwe mimi na kunyongwa lakini wewe uwe huru
nakupenda mno mama!” Alisema Prosper huku akilia.
Baada
ya maongezi Prosper alirejea mjini ambako alikwenda moja kwa moja kituo cha
polisi kati mjini Tabora.
“Naomba
kuonana na mkuu wa kituo!”
“Wewe
nani na una shida gani?”
“Nina
maongezi marefu kidogo siwezi kukueleza wewe!”
Alionyeshwa
ofisi ya mkuu wa kituo na kuingia.
“Shikamoo
mzee!”
“Marahaba
nikusaidie nini kijana!”
“Mzee
unakumbuka mzee Kabaka aliyeuawa siku chache zilizopita?”
“Ndiyo
si yule aliyeuawa na mke wake?”
“Ndiyo!
Yule ni baba yangu na aliyemuua si mama yangu ni mimi! Nilitoroka baada ya
kitendo hicho na ninakueleza wazi kuwa nimerudi ili mama yangu aachiwe mimi
ndiye niwekwe rumande!”
“Kweli?”
“Huo
ndio ukweli ni mimi niliyempiga baba na mchi kichwani akafa!”
“Kwanini?”
“Kwa
sababu alikuwa anamtesa mama yetu!”
“Mungu
wangu!Afande Charles!”
“Naam
Afande!”
“Hebu
njoo hapa mara moja!”
Sekunde
tano tu tayari askari alisimama mbele ya meza ya mkuu wa kituo.
“Ndiyo
afande!”
“Mchukue
huyu kijana umpeleke rumande, kumbe ndiye aliyemuua baba yake kule Tutuo na
sisi tukawakamata mama yake na dada zake sasa amejileta mwenyewe! Peleka
mahabusu haraka na mama yake na dada zake waachiwe mara moja”
“Sawa
afande!”
Askari
alimnyanyua Prosper na kumzaba vibao kadhaa usoni, kisha akamchukua +255 758
018 597 whatsapp. +255 758 018 597
Nafahamu wewe ni msomaji mzuri wa simulizi zetu na unatuamini sana, zaidi tumependa kukuletea huduma ya ENGLISH COURSE kwa njia ya online na uso kwa uso kama upo dar es Salaam (+255 758 018 597).
0 Comments
Karibu sana, tuma ujumbe whatsapp +255 758 018 597 kujipatia simulizi zetu
Emoji