Pigo Matata (Riwaya) - Kijasusi



KAMANDA Amata alikuwa kachanganyikiwa akili kwa namna moja au nyingine, alikuwa akiona kama ndoto inayotokea mbele yake, hakuamini kama wamewahiwa namna hiyo na kwa kasi ya ajabu, alijiuliza kila wakati ni nani mwenye uwezo wa kuwanasa namna hiyo, hakupata jibu zaidi ya hapo aligundua kuwa kwa vyovyote ni watu hatari wanaojua nini wanafanya na kwa wakati pia alielewa watu hao wamepewa kazi kwa muda maalumu hivyo na yeye kama ilimpasa kuwa saidia wenzake alitakiwa ajipe muda maalum na muda wa kazi yake uwe mdogo kuiko muda wa adui zake pia ucheze ndani ya muda wa adui zake. Alitikisa kichwa kana kwamba kuna mdudu akimtembea kwenye ubongo wake, akaitazama saa yake, saa zinayoyoma kwelikweli.
Ilikuwa inakaribia saa nane usiku alipokuwa akifungua geti la nyumbani kwake, akaingia na kulifunga nyuma yake, kisha akasimama kidogo kuangalia nini kinaendelea huku na kule, kwa macho yake makali aliweza kuona ua moja kubwa likitikisika kidogo, akaelewa wazi kuwa mtikiso huo lazima kuna kitu na si wa upepo kwani hali ya hewe ilikuwa imetulia sana na haikuwa na upepo. Damu ikamtembe haraka mwilini, hakufanya lolote, akauendea mlango wa nyumba kubwa na alipoufikia alikuta karatasi iliyoning’inizwa mlangoni, kisu chembamba chenye makali kuwili kilitumika kuishikia hiyo karatasi pale mlango.
Mwisho wa zama zenu umefika, mtaongea na Ngurumo.
Ulikuwa ujumbe uliosomeka katika karatasi hiyo pale juu. Akakikamata kile kisu na kukichomoa kwa nguvu, akakibusu, akaiokota ile karatasi na kuishika mkononi kisha akaingia ndani na kuuacha mlango wa nyumba yake bila kuufunga makusudi tu. Moja kwa moja akakiendea chumba chake na kufungua kabati kubwa lililokuwa mbele yake. Akavuta fulana yake nyeusi kaba shingo ya mikono mirefu akaivaa ikitanguliwa na vesti nyeusi pia. Kizibao cheusi chenye mifuko mingi ya kuwekea zana mbalimbali kikafuata juu yake, na zana zake zikapachikwa, bastola nne zilizosheheni risasi zikakaa mahala pake, visu vidogodogo vikawekwa mahala pake, paketi za risasi zikawekwa mahala pake, Shotgun mbili zikabanwa mahala pake nazo zikiwa zimetimia. Akakusanya vikolokolo vya kutosha kwa pambano hilo ambalo hakujua ni nani haswa anakwenda kupambana naye.
Akiwa kasimama kwenye kioo, anajiweka sawa, akahisi vinyweleo vyake vikisimama, mwili ukamsisimka, akajua kuna jambo, akalisubiri huku akijifanya hajui lolote.
Palepale kwenye kioo alimuona mtu akiingia kwa minyato kumfuata, Kamanda alitamani kucheka kwa sababu hata kama alikuwa akinyata wakati yeye alikuwa akimuona kwenye kioo ni kazi bure. Akamsubiri amkaribie ili ajue nini cha kumfanya. Yule mtu akajiandaa kwa waya aliokuwa kaufunga kutoka mkono hu mpaka ule mwingine.
Anataka kunikaba, Kamanda akawaza. Kisha kwa kasi ya ajabu akageuka na guu lake lenye nguvu likatua kichwani mwa Yule mtu, akajibwaga na kujibamiza kwenye mwamba wa kitanda, yowe la maumivu likamtoka, kabla hajafanya lolote akamnyanyua na kumpa kichapo kikali, alipohakikisha kuwa hali aliyokuwa nayo hawezi fanya lolote akamkalisha chini na kumwegemeza ukutani, akamtikisa na kumtazama usoni.
“Nani bosi wako?” akamwuliza.
“Si-si-simjui!” akajibu kwa tabu.
“Unaniletea utani siyo?” akamwuliza kwa ukali.
“Kweli simjui, mi natumwa tu na kulipwa ujira mkubwa wa kunitosha, kwa hali ya nchi yetu nakubali kufanya kazi yoyote kwa malipo yoyote,” akajieleza.
“Nafikiri hunijui sawa sawa sasa utanijua!” Kamanda akamwambia kisha akamkamata korodani zake na kuziminya kwa nguvu.
“Aaaaaiiiiggggghhhh…. Niache, niache nitasema,” akalia kwa uchungu.
“Sema, nani bosi wako, nani aliyekutuma kuja hapa?” kamanda akauliza sasa kwa ukali zaidi.
“Kweli kaka sim-ju-jui…” akajibu huku akijigeuza geuza.
Kabla Kamanda hajauliza linguine, akashuhudia povu jeupe likitoka kinywani mwa Yule mtu.
“Shiiit! Limejiua,” akang’aka kwa sauti, akaanza kumpekua.
Katika moja ya mfuko wa suruali yake akatoa simu ya mkononi, zaidi ya hapo hakuona chochote cha maana. Akaitazama ile simu, akaenda kwenye kitabu cha majina akakuta majina matano tu, la kwanza kabisa likamvutia, lilikuwa limeandikwa kwa jina moja tu ‘Naima’, kisha akaliangalia la pili na la tatu. Akaamua kuanza kampeni na jina hilo la kwanza.
Akaperuzi upande wa ujumbe mfupi, akakutana na ujumbe kutoka kwa Naima uliotumwa ndani ya dakika kumi zilizopita lakini ulionekana kutojibiwa.
‘…Akifika nijulishe nije nimalize kazi…’ ujumbe ulisema hivyo.
Lilifikiri litaniweza, sasa naanza na Naima, kawaza na kuamua kuujibu ule ujumbe.
Kamanda Amata akaujibu ule ujumbe, kisha akaburuza mwili wa Yule mtu na kuubwaga katika mlango wan je kisha yeye akalitoa pikipiki lake na kuliegesha nje kabisa, akisubiri kuona kinachoendelea.
Akiwa nje ya nyumba yake, juu yapikipiki lake kubwa akasubiri kimya nje kabisa ya nyumba yake.
Dakika tano hazikupita, mwanga wa taa za gari ukaonekana ukijitokeza katika kona ya barabara na kuelekea mtaa huo ilipo nyumba ya Kamanda Amata. Ilikuwa Ford Ranger nyeusi, haikuwa na namba za usajili, ikasoge polepole na kuegeshwa karibu kabisa na lango la nyumba hiyo, watu watatu wakashuka, mmoja kati yao alikuwa mwanamke, alionekana ndiye akiongoza wengine, aliwapanga, mmoja alimwamuru abaki langoni, yeye na mwingine aliyeonekana pande la jitu waliingia ndani.
§§§§§
Naima na lile jitu moja kwa moja waliingia getini na kutembea kwa minyato huku silaha zikiwa mikononi mwao. Wakiwa wanajigawa kiufundi zaidi kuuelekea mlango, walishangazwa na ukimya uliotawala, lakini hawakujali. Lilikuwa ni lile pande la mtu lililotangulia kuuendea mlango, kabla halijafika likajikwaa kwenye kitu kama gogo.
“Aah!” likajivuta na kujibwaga mbele. Lilipogeuka nyuma likaona mwili wa binadamu, “Shiit! Amemuua,” akasema kwa sauti.
“Nani amemuua?” Naima akauliza, kisha akashusha silaha yake na kusogea pale ulipo ule mwili, akaugeuza, na kuchomoa kijikaratasi kilichopachikwa kinywani mwa marehemu.
…Naanza na wewe…
Naima akageuka huku na kule asione mtu, anaanza na mimi! Hata kama Naima alikuwa ni muuaji mzuri kitaaluma lakini alijikuta akishikwa na ubaridi wa ghafla. Wakaingia ndani wakatafuta huku na kule hawakuona mtu zaidi ya redio kubwa iliyokuwa ikipiga muziki laini wa ‘Killing me softly’ akasonya na kutoka nje. Wakabeba mwili wa mwenzao na kutoka nao.Wakaubwaga katika nyuma ya pikap yao na kufungia. Kisha nao wakaingia garini na kuondoka.
§§§§§§
Kamanda Amata akawasha pikipiki lake, bila kuwasha taa, akaingia barabarani na kuwafuata taratibu, wakaikamata barabara ya Kinondoni na kuvuka daraja la Salenda kisha wakaelekea mjini, moja kwa moja mpaka Mbowe Club, wakaegesha gari na kuteremka kisha wakapotelea ndani.
Kamanda Amata akaingia baada yao na kuhakikisha hawapotezi katika himaya ya macho yake, akaketi katika moja ya viti vya kaunta na kuagiza glass moja ya Whisky akachanganya na sprite baridi kisha akawa anakunywa taratibu.
Wale jamaa wakaketi mahala Fulani wakijadiliana jambo lakini wakionekana kuwa na wasiwasi, kila mara Naima alionekana kuisoma ile karatasi na kuiweka tena mfukoni. Mara lile jitu la miraba mine likanyanyuka na kutoka mahala pale likamwacha Naima na mwingine mmoja. Kamanda Amata alipogeuka hakuliona lile jitu limeingilia kona gani, akili yake ikazunguka mara mbili, akateremka katika kile kiti na kujichanganya katikati ya watu waliokuwa wakiburudika na uziki katika ukumbi huo. Dakika kadhaa baadae akaliona lile jitu pale kaunta likinga’aang’aa macho, likabeba vinywaji na kuelekea kule lilikokaa tangu mwanzo, yote hayo Kamanda Amata alikuwa akiyatazama kutoka katika kundi la watu wale. Alipoona kuwa hakuna aliye na yeye alirudi tena kaunta na kuagiza kinywaji, lakini hakuweza kukimaliza baada ya kumwona Naima akinyanyuka kitini na kuelekea nje, Kamanda Amata naye akatoka na kumfuatilia mwanadada huyo.
Naima alisimama kati ya magari na kuweka simu yake sikioni kisha akaendelea kuongea na aliyekuwa upande wa pili.
Naima akiwa anaendelea kuongea na simu alihisi ubaridi ukimgusa maeneo ya shingoni, akashtuka akataka kugeuka.
“Tulia!” sauti nzito ya Kamanda Amata ikapenya sikioni mwake. Naima akatulia kama alivyoamuriwa, “Nilikwambia nitaanza na wewe, na ndiyo sasa naanza,” akaongeza.
“Weweni nani?” Naima akauliza kwa sauti yake nyororo inayoweza kumnyong’onyesha mwanaume yeyote Yule rijali.
“Mimi ni Yule mnayenitafuta, Kamanda Amata, na nataka unambie watu wangu wako wapi?” Kamanda akaongeza swali kisha akatulia. Naima naye alitulia bila kujibu, akitafakari la kufanya. Baada ya sekunde kadhaa, uamuzi aliofuanya haukuwa mzuri hata kidogo. Aligeuka na pigo kali kwa Kamanda Amata, lakini Kamanda aliliepa kiufundi huku bastola yake ikimtoka mikononi. Naima aliruka sarakasi kwa minajiri ya kuiwahi le bastola lakini kabla hajafika alijikuta akipokea teka la nguvu mbavuni na kutupwa upande wa pili, akajiinua haraka na kusimama wima kumkabili Amata. Amata alijiweka sawa mwili wake na kumwendea kama mbogo, Naima alijiweka sawa na kuvamiana na Amata, kama Kamanda alifikiri mwanamke huyo anapigika kirahisi alikosea, mapigo matatu ya haraka yalimwingia Kamanda akajikuta anapoteza netweki, akajaribu kujitutumua lakini akajikuta amedhibitiwa ka mikono imara ya mwanamama huyo.
Naima alijirusha hewani kama jani la mkorosho na kuachia dabo kiki za maana zilizotua sawia kifuani mwake na kumpeleka chini.
Kisha Naima akatua chini kwa miguu miwilia akimtazama Kamanda Amata akigalagala chini.
“Ha ha ha ha niliambiwa kuwa Amata ni mwanamume wa chuma kaa mbali naye! Chuma kiko wapi hapa? Na sasa nakuua kwa mkono wangu kwani nimeahidiwa pesa nyingi sana kama roho yako nikiipeleka kwa bosi wangu,” Naima aliongea kwa kujiamini huku akiiweka sawa mikono yake tayari kumshushia pigo la mwisho kijana huyo. Alipomjia kumvamia alimshuhudia Kamanda Amata akijirusha kutoka chini kwa mtindo wa ajabu na guu lake la kulia likatua chini ya kidevu cha Naima, akanyanyuliwa na kubwagwa upande wa pili meno kadhaa yakimtoka.
“Mpo chini ya ulinzi!” sauti kali ikasikika upande mwingine. Kamanda alipotupa jicho akaona polisi eneo hilo, akaruka sarakasi na kutua upande wa pili wa gari, akajibana sehemu ambayo kutokana na nguo zake hakuweza kuonekana, akitazama linaloendelea.
Amata alishuhudia wale polisi wawili wakichezea kichapo…. Whatsapp +255 758 018 597


Post a Comment

0 Comments