Daktari Mtata (Riwaya) - Utamu 18+



“Ulikwenda hospitali mke wangu?” Masofa alimuuliza mke wake Sulee.

“Nilikwenda, lakini daktari kasema mimba nitapata tu ndani ya mwezi mmoja.”

“Ndani ya mwezi mmoja utapata mimba? Inawezekana kweli? Hujamwambia kwamba tumehangaika kutafuta mtoto kwa miaka nane, sasa ndani ya mwezi mmoja mimba itapatikana vipi?”

“Mimi sijui Masofa.”

“Mh! Haya, kwa sababu tumeambiwa na mtu tunayemwamini tuangalie, labda kweli daktari yule atatusaidia. Hakusema uende na mimi?”

“Hakusema Masofa, ila alisema kama naweza kesho na keshokutwa niende usiku saa moja ili anipime vizuri.”

“Alikupa dawa?”

“Dawa atanipa kesho.”

Masofa alichukua simu akampigia rafiki yake Miraji…

“Ee bwana Miraji, yule dokta uliyemsema kasema ‘waifu’ aende kesho saa moja usiku, wewe si unamwamini?”

“Yule hana neno, aende tu. Bwana Masofa we hukumbuki jinsi mimi na shemeji yako tulivyohangaika kutafita mtoto?”

“Nakumbuka.”

“Sasa kama si huyo daktari wa wanawake unadhani tungepata mtoto?”

“Oke, nimekuelewa bwana Miraji.”

“Sawa Masofa.”

Masofa alikata simu, akaendelea kukaa chumbani. Akili yake ilikuwa nzito sana kumruhusu mkewe arudi hospitali kesho yake, tena usiku wa saa moja…

“Sasa huyo daktari wa watoto ni kwa nini anataka mke wangu arudi usiku? Ni tiba gani hiyo ya usiku wa saa moja?”

***

Siku ya pili iliingia, saa moja jioni Sulee alikuwa kwa daktari wa wanawake anaitwa Dokta Kisarawe.

Dokta Kisarawe alikuwa amekaa ndani ya chumba cha utabibu kwenye zahanati yake huku akimwangalia Sulee kwa macho yenye huruma…

“Kwa hiyo tatizo kubwa ni mtoto tu anti yangu?”

“Ni mtoto tu.”

“Miraji unamjua?”

“Ndiyo, ni rafiki wa mume wangu Masofa kwani vipi dokta, mbona umemtaja huyo?”

“Ah! Nimeangalia kwenye maelezo yako, nikagundua kuwa mnatoka eneo moja kwa maana ya ubalozi…,” Dokta Kisarawe alijibu huku akimuangalia Sulee kwa macho ya kumkagua f’lani hivi.

“Ooh…!, maana nilishangaa ni kwa nini umuulize huyo na umejuaje kama ninafahamiana naye…,” Sulee alihoji huku akiyakimbiza macho yake pembeni baada ya kukutanisha na ya Dokta Kisarawe.

“Hata mkewe alikuwa na tatizo kama la kwako, lakini aliponea kupitia mikono hiihii…”

“Kweli dokta…?”

“Kweli nakuambia, niamini mimi.”

“Mm!, sawa lakini nimesumbuka sana kwani naumia kukosa mtoto jamani…,” alisema Sulee safari hii akionesha sura ya upole zaidi, hali iliyomfanya Dokta Kisarawe amkazie macho zaidi.

“Kwani mmehangaika kwa muda mrefu sana anti…?”

“Yaani wee acha tu dokta, ikishindikana na hapa itabidi niridhike tu kuwa sikupangiwa kuzaa kabisa…”

“Ndoa yenu ina muda gani sasa…?,” Dokta Kisarawe alizidi kumdadisi Sulee huku muda nao ukizidi kuyoyoma na tayari saa iliyokuwa ukutani ilisomeka saa mbili na dakika nne.

“Miaka mitatu sasa dokta…”

“Mm..!”

“Mbona unaguna dokta jamani, au huamini?”

“Hapana anti, naguna kwa kushangaa mwanamke mzuri kama wewe hujapata mtoto…!,” alijibu Dokta Kisarawe huku akimkazia macho Sulee hasa maeneo ya kifuani na mapajani kutokana na sketi aliyokuwa amevaa kupanda hadi kuvuka juu ya magoti.

“Kwani mimi mzuri ja..ma..ni…?,” aliuliza Sulee lakini safari hii kwa sauti iliyokatakata.

“Dah! Wewe ni mzuri sana anti, nashangaa hadi sasa hujapata mwanaume wa kukupa mimba…!”

Hapo Sulee hakusema neno zaidi ya kuendelea kumtumbulia macho Dokta Kisarawe aliyekuwa bize na kumungalia.

Alipoona Sulee yuko kimya, Dokta Kisarawe akazidi kumsifia huku akimhakikishia ni lazima atapata mimba.

“Yaani mwanamke umeumbika haswa, ona maeneo kama haya ya kifuani jamani…,” Dokta Kisarawe aliendelea kumchombeza Sulee huku sasa akionesha kwa vitendo na kuyagusa maeneo ya kifuani ya mwanamke huyo mrembo wa sura na umbo achilia mbali rangi yake ya chokoleti.

“Kwe…kwe…lii dokta jamani…?,” Sulee aliuliza kama kweli anaweza kuzaa lakini kwa sauti ya mkwamo kutokana na mkono wa dokta kugusa maeneo nyeti ya kifuani.

“Duh! yaani anti na nido nzuri kama hizi halafu huzai…!”

“Mm!,” Sulee aliishia kuguna huku akijikunja kiaina kwani safari hii vidole vya dokta viligusa kisawasawa nido zake kutokana na blauzi nyepesi aliyoivaa mwanamke huyo.

“Hujapata tu mwanaume rijali…”

“Kwanini unasema hivyo dokta jamani…,” Sulee aliuliza katika hali ya kutojiweza, huku macho yake yakianza kubadilika rangi na kuwa mekundu kiasi.

“Mimi ni daktari si kwa matokeo ya mtihani bali kwa kukidhi vigezo, ina maana nina uwezo wa kujua tatizo la mgonjwa hata kwa saikolojia tu, yaani wewe unahitaji mwanaume rijali tu, kweli tena nakuambia,” Dokta Kisarawe alizidi kutoa maelekezo kwa vitendo zaidi na safari hii mikono yake ikiparaza juu ya mapaja ya Sulee.

“Aah! Sasa huyo mwanaume rijali nitampata wapi jamani mbona haya ni majaribu sana dokta…?”

“Kha! Mbona wapo wengi sana, huko mitaani au hata mimi…”

“Mimi wa mitaani naogopa, mume wangu ni mkorofi sana…”

“Basi mimi…,” Dokta Kisarawe alipasua ukweli wake huku mikono yake ikiwa na kazi ya kumpapasa na kumbinya kimtindo Sulee, kuanzia maeneo ya kifuani, mapajani hadi mgongoni na kumalizia kwenye kiuno kipana na cha mviringo cha mwanamke huyo.

Kutokana na joto la mikono ya dokta, Sulee alikuwa akipeleka upinzani hafifu na kuruhusu mikono hiyo izidi kutalii kadri iwezavyo na kumuacha akilalamika kimahaba huku akitamka maneno ya kukolea penzi.

“Aaah, jamani dokta lakini mimi siumwi huukooo…,”

Whatsapp/Call  - +255 758 018 597 utatumiwa muda huu



Post a Comment

0 Comments