Whatsapp 0758 018 597 Usiku wa siku hiyo, Os Anjelus hakupata usingizi aliouzoea kule alikohama. Ni kawaida, watu wengi hukosa mtiririko mzuri wa usingizi wanapolala eneo geni… |
“Iko haja
ya kumwita mke wangu sasa. Si nilimpeleka nyumbani ili nitafute chumba kingine?
Si nimeshakipata? Sasa nini tena?
“Lakini
loh! Yule mama mwenye nyumba kule nilikohama kiboko. Mama mdomo mchana kutwa!
Uchafu kidogo wa kuufagia sekunde kumi yeye anafoka nusu saa? Sijawahi kuona
mimi.
“Sasa kwa
mfano siku ile alipotupa notisi kwa ule uchafu wa kuufagia dakika mbili tu kama
nisingemtishia kwenda polisi, si angeongea siku nzima?” aliwaza Os Anjelus huku
akihisi kizunguzungu cha ugeni, lakini msisitizo wake mkubwa ndani ya moyo ni
kumwita mkewe, Happy.
***
Asubuhi
kulikucha, Os Anjelus alikuwa wa pili kutoka nje. Wa kwanza alikuwa mama Tina,
baada ya yeye ndiyo akatoka Halima ambapo alimtengea maji ya kuoga mwanaume
aliyerudi naye usiku uliopita.
Ilikuwa
mara ya kwanza kwa Halima kuonana uso kwa macho na Os Anjelus kiasi kwamba, mwanzoni
Halima alijua ni mgeni wa mama Tina…
“Za leo
anko?”
“Nzuri
sista, mzima wewe?”
“Mzima,
karibu sana.”
“Asante
nimekaribia.”
Lakini
Halima hakumuuliza Os Anjelus kama yeye ni nani kwenye nyumba ile, aliogopa
kuonekana ni ‘mshankupe’ wa mtaa.
Kila mmoja
aliendelea na lake, Os Anjelus aliingia chooni, Halima alitenga maji akaenda
ndani kumwita jamaa yake, anaitwa Mabange.
***
Halima
alitoka na Mabange kwenda kwenye saluni yake, kwenye korido akakutana na mama
Tina…
“Za asubuhi
mama Tina?”
“Nzuri
Halima, umeamkaje?”
“Salama
tu,” alisalimia Tina, akapunguza sauti…
“Eti huyu
kijana ni nani, mgeni wako?”
“Mgeni
wangu?! Aka! Si mpangaji mpya aliletwa na mwenye nyumba juzi.”
“Ooo, kwa
sababu sikuwepo. Anafanya kazi wapi?”
“Mi sijui
Halima.”
“Ana mke?”
"Halima,
mimi sijui lolote."
"Ana
gari?"
"Halima
bwana, mi sitaki," alisema mama Tina huku akiondoka kwa mwendo wake wa
madaha.
Halima
aligeuka kumwangalia huku akimtamani maana japokuwa ni mwanamke mwenzake lakini
moyoni amekuwa akikiri kwamba, mama Tina aliumbika kuliko yeye.
Mama Tina
alijaliwa. Kwenye bodi nyuma alikuwa amefungashia, kiuno kilikatika vizuri,
japokuwa alishazaa mtoto mmoja lakini bado nido zake zilikuwa zinadai kama za
binti aliyeingia ukubwa.
Mviringo wa
miguu yake na kuitwa jina la bia lilimfanya azidi kutamanika hata machoni pa
wanawake wenzake. Sura yake ilijaliwa duara lenye upole na macho ya kulewa huku
midomo ikishibishwa na unene wa rangi nyeusi.
Sauti ya
mama Tina ilikuwa na uwezo wa kuwafanya wananchi wenye hasira kali wamsamehe
kumchoma moto kibaka aliyemkwapulia simu mzee maarufu wa mtaa.
Siku
mojamoja, hasa Jumapili alipokuwa akienda kanisani, aliwaacha hoi watu wa
mtaani kutokana na magauni yalivyokuwa yakimkaa.
Umri wake
wa miaka 32 ulimtosha kuendelea kuonekana msichana mbichi kutokana na kujitunza
na kujaliwa ngozi nzuri na Muumba.
***
Asubuhi
iliyofuata, Os Anjelus alitoka chumbani kwake na kukutana na mama Tina kwenye
korido
"Za
asubuhi anko?"
"Nzuri
anti, umeamkaje?"
"Salama
tu. Naona kumekucha?"
"Ee,
kumekucha anti, nataka kufua kwanza halafu ndiyo niende kibaruani."
"Pole
sana. Ungetafuta mtu wa kukusaidia kazi kama hizo anko."
"Ni
kweli, unajua nina mke lakini yupo kwao, nadhani mwisho wa mwezi huu
atakuja."
"Hapo
itakusaidia."
Mazungumzo yao
yalitumia kama dakika moja, kila mmoja akaendelea na mambo yake.
Baba Tina
aliondoka kwenda kazini, Os Anjelus alikuwa amemaliza kufua na sasa alikuwa
akijiandaa kwa kutoka
"Ngongo;ngo,"
mlango wake uligongwa.
"Karibu,"
alisema kijana huyo huku akifungua mlango
"Oo
anti, karibu."
Mama Tina
mkononi alishika sinia lenye chupa ya chai, sukari, kikombe na vitafunwa
"Karibu
chai anko."
"Ooo.
Anti mbona unasumbuka jamani?"
"Usijali
anko, we kunywa tu."
"Asante
sana."
Os Anjelus
alipokea sinia hilo na kurudi ndani kwake, akanywa chai na kurudisha vyombo
"Anti
vyombo hivi."
Mama Tina
alitokea, akapokea sinia lake huku akishukuru
"Baadaye
basi anti."
"Sawa
anko, nilikuwa na wazo moja anko. Ungeacha funguo nikufanyie usafi chapuchapu."
"Hapana
nitafanya mwenyewe anti, nisikusumbue."
"Noo,
hunisumbui anko, we acha tu."
"Jamani,
nitakuchosha anti."
"Wala
ndiyo kazi zetu akina mama tukiwa nyumbani."
Os Ajelus
aliacha funguo, mama Tina akaipokea na kuifunga kwenye pindo la khanga aliyovaa.
Nusu saa
mbele, mama Tina alikuwa ndani ya chumba cha Os Anjelus akifanya usafi. Baadhi
ya vitu havikuwa vimepangwa, akapanga yeye alivyoweza huku moyoni akimsifia
kijana huyo kwa kuwa na vitu vizuri na vya kisasa.
Alibabaika
zaidi kwenye kitanda na mashuka. Ilifika mahali alijitupa kitandani na
kunesanesa huku moyoni akisema
"Kinaonekana
kinatoa usingizi mnono."
********************************
"Nimekuletea
chakula anko," mama Tina naye alitumia sauti ya chini.
"Da!
Asante sana anti."
Wakati Os
Anjelus anapokea, sauti ya Halima mlangoni ilibisha hodi
"We
kaka wa Kingoni."
Ukimya
ulitawala kwa muda kwani Os Anjelus alishindwa kuitikia kutokana na uoga kwamba
angeingia angemkuta mama Tina
"Wenyewe
humu ndani, hodini," alikomaa Halima.
"Sikia,
nenda, fungua mlango lakini usimruhusu aingie ndani hata sekunde moja,"
mama Tina alimwambia Os Anjelus kwa sauti ya chini sana ili asisikie Halima
kule mlangoni.
"Sawa,"
Os Anjelus alikubali huku akienda kufungua mlango. Mama Tina akijibana kwenye
kona ya chumba ili asionekane maana mlangoni hapakuwa na pazia.
"Vipi
we Mngoni, mzima?"
"Mzima
dada angu, karibu sana."
Mama Tina
kule ndani aliposikia karibu sana, alishtuka sana, alijua kijana huyo
atamruhusu Halima apite kuingia
"Mwenzetu
ujio wako kufahamiana ni muhimu, ulikuwa ukiishi wapi zamani?"
"Mburahati."
"Una
mke?"
"Nina
mke na mtoto mmoja."
"Wako
wapi sasa?"
"Wako
kijijini."
"Watakuja
lakini?"
"Mwisho
wa mwezi huu watakuwa hapa."
"Sawa,
sasa unakula nini maana napika."
"Hapana
anti, usijali kuhusu suala la chakula, mi tayari."
"Kwani
unapika humu ndani?"
"Nakula
gengeni."
"Hivi
hiki chumba ni kikubwa kweli?" Hebu nione ndani," Halima alisema
akionesha dalili za kutaka kuingia kwa kuinua mguu mmoja na kukanyaga mbele.
"Sista
samahani, iko siku utaingia lakini si leo," alisema Os Anjelus huku
akiinamia chini kwa aibu.
"Yaani
mimi kuingia kwako anko mpaka unipangie siku, unajua ni kwa kiasi gani
nimekupenda?" Halima alipasua jipu kwa mara ya kwanza
"He!"
kule ndani mama Tina alijikuta akisema kwa sauti ya mshangao
"Yaani
mwanamke anajitongozesha hivihivi, ama kweli Halima ni malaya sana
jamani," alisema mama Tina lakini huku mapigo ya moyo yakimwenda kwa kasi.
"Sista
utanipendaje wakati nimekwambia nina mke wangu? Mimi hapa ndani hakuna mwanamke
nitakayetembea naye kwa sababu kati ya mambo siyataki ni pamoja na
usaliti."
"Ina
maana hujawahi kumsaliti mkeo?"
"Na
wala sina wazo hilo."
"Basi
mwenzetu kumbe ana bahati ya mtende, kuota jangwani."
Mama Tina
alimsifia kijana huyo, hasa kwa msimamo wake aliouonesha kwa Halima kwamba
hawezi kumsaliti mke wake.
Halima
aliondoka, Os Anjelus akafunga mlango kwa funguo na kurudi, akakaa kitandani
huku akimwangalia mama Tina kwa macho ya huruma kwa jinsi alivyokuwa amejibanza
kwenye kona
"Pole
sana anti."
"Usijali
anko, kawaida tu. Unajua huyu msichana ana mdomo sana, angeniona hapa
angekwenda kuyatangaza nje."
"Ni
kweli kabisa, umetumia busara kushauri asiingie."
"Sasa
mi nitatokaje humu?" alihoji mama Tina.
"Ngoja
nitoke mimi niangalie hali ya hewa."
"Sawa."
"Mama
Tina," aliita Halima kule nje..
"We
mama Tina."
Mama Tina
aliogopa zaidi, alijua Halima ataingia kwake na atamkuta mtoto. Na ikawa hivyo
kweli
"We
Tina mama yuko wapi?"
"Katoka."
"Kaenda
wapi?"
"Sijui,
aliweka chakula kwenye sufuria akatoka."
Tina alijua
hotipoti ni sufuria.
Halima
alishtuka kusikia mama Tina aliondoka na sufuria yenye chakula
"Kaenda
nacho wapi? Atakuwa kampelekea yule kijana."
***
Wiki moja
tu mbele, siku hiyo mama Tina alikuwa akitoka gengeni, akakutana na mama mmoja
jirani yake anaitwa mama Sindilia.
"Nilikuwa
nakutafuta sana mama Tina."
"Kuna
nini tena mama Sindilia."
"Mwenzangu
si umbeya wa mtaani, uhujui?"
"Upi
huo mama Sindilia."
"Nasikia
unatembea na kijana mpangaji mwenzenu ndani."
"Eti
nafanyaje?"
"Nasikia
kuna kijana mmoja kahamia kwenu, ndiyo unatoka naye. Nikasema mama Tina
huyuhuyu ninayemjua mimi anaweza kufanya upuuzi huo kweli?"
Ha!
Mama Sindilia, unavyoona naweza kufanya upuuzi kama huo kweli, mimi mama Tina?
Na ndoa yangu tamu?"
"Ndiyo
nikashangaa. We hujasikia?"
"Sijasikia
kokote."
"Basi
kaa ujue hivyo."
"Wewe
nani kakwambia?"
"Mh!
Mwenzangu hayo mengine sana, tutaonana siku nyingine," alisema mama
Sindilia huku akiondoka zake.
Mama Tina
nusura presha impande kwani watu wa mtaa ule anawajua vizuri, si ajabu
kumwambia mume wake kuhusu tetesi hizo jambo ambalo litamuweka pabaya.
"Hivi
atakuwa nani? Au Halima? Huyu atakuwa Halima tu," alisema moyoni mama Tina
wakati akiingia nyumbani kwake.
Licha ya
kuwepo kwa madai hayo, mama Tina alitafuta muda wa kuonana na Os Anjelus ili
amsimulie habari za mtaani.
Ilikuwa
wakati kijana huyo amerudi, kabla hajaingia kwake, mama Tina alimdaka kwenye
korido
"Anko
kuna kitu kikubwa sana na cha hatari kinataka kutokea."
"Kinahusu
nini anti?"
"Mimi
na wewe."
"Nini
tena anti?"
"We
nenda, usifunge mlango nitakuja kukwambia."
"Poa."
Os Anjelus
alizama chumbani mwake, akapumzika kidogo kisha akatoka kwenda kuoga, aliporudi
alivaa bukta tu na kujitupa kitandani huku akiwa amefungulia feni kwa spidi ya
kawaida.
Mama Tina
alimalizana mambo yake, akatembea kuelekea kwa kijana huyo huku akiwa katika
hali ya tahadhari. Kabla ya kuingia alimpigia simu Halima akiwa amesimama usawa
wa mlango wa chumba chake
"Halina
leo unarudi saa ngapi nataka kukuagiza kitu."
"Mh!
Kusema ukweli nitachelewa sana, kuna sehemu nitakwenda kujirusha, labda kwenye
saa sita, saba usiku. Ulitaka kuniagiza nini?"
"Sabuni."
"Labda
nikununulie nikupe asubuhi."
"Hapana,
nitakwenda kununua pale kwenye duka la urembo la kisimani."
"Poa."
Mama Tina
akaondoa wasiwasi, maana alidhani Halima angeweza kuingia muda wowote ule.
Alizama ndani kwa Os Anjelus.
"Vipi,
naona umelala?"
"Nimepumzika
tu anti, si unajua tena."
"Ni
kweli," alisema mama Tina akikaa pembeni ya kitandani, akashika godoro
kulia na kushoto kama anayetaka kuaga kuondoka.
"Mwenzangu,
leo nimekutana na mama mmoja jirani, akasema amesikia eti mimi natembea na
wewe, he! Nilishangaa sana, mimi sijawahi kupata kashfa kama hiyo hata siku
moja katika maisha yangu ya ndoa."
"Mh!
Kweli? Yeye huyo mwanamke alisikia wapi?"
"Kagoma
kuniambia, lakini mimi nahisi Halima."
"Halima
yupi, huyu dada wa chumba cha pili?"
"Huyohuyo."
"He!
Mbona anataka kuleta balaa."
"Balaa
balaa, tena ni uuaji, maneno kama hayo yakifika kwa mume wangu si ndoa
sina!"
"Kabisa
anti. Dah! Ni wa kumwonya lakini."
"Mh!
Mimi sitamwambia kitu, ila Mungu atanilipia, iko siku yake. Mi najua anakutaka
ndiyo maana anafanya hivi, yeye anadhani mimi na wewe ni wapenzi," sasa
mama Tina alianza kupunguza sauti. Akaendelea
"Tena
naomba anko, isije ikatokea hata siku moja umekaa naye ukasema ninavyokusaidia
kusafisha nyumba au kukupa chakula
"Anti,
mi si mtoto, siwezi hata siku moja
"Unanihakikishia
anko?"
"Kweli
kabisa."
"Mh!
Tushikane mikono tule kiapo."
Os Anjelus
akatoa mkono, mama Tina akaupokea, akaubana;
"Ukikiuka
itakula kwako."
"Siwezi
kukiuka."
"Kweli?"
"Kabisa."
"Siamini,"
sasa mama Tina alimsogelea usoni kijana huyo;
"We
amini."
"Nifanyie
kitu chochote niamini," alisema mama Tina.
"Unataka
nikufanyie kitu gani?"
"Chochote
ambacho mimi nitaamini kweli hutaweza kuanika siri yetu."
Os Anjelus
akashtuka,
Fika
whatsapp +255 758 018 597 (1000Tsh utaipata ikiwa kamili)
Instagram @kulayasimulizi
0 Comments
Karibu sana, tuma ujumbe whatsapp +255 758 018 597 kujipatia simulizi zetu
Emoji