Riwaya - Kinasika Damshi (18+)


"Yani na leo nisingekukuta, ningeumwa ugonjwa ambao kuutibu ungehitaji gharama kubwa" alikuwa ni Emmy akiongea maneno hayo bila kujali wateja waliokuwa pale. "Usijali maadam umenikuta kila kitu kitakuwa sawa" nilimjibu. Hata wateja walipoisha na kubaki sisi wenyewe, Emmy hakuwa na la maana aliloliongea zaidi ya kujichekeshachekesha. Hakukaa sana, akaniomba namba yangu. Alipofanikisha hilo akatuaga na kuondoka. Mwili wangu ulikuwa nyang'anyang'a kwa uchovu. Hata kuwepo kazini ilikuwa kujilazimisha tu. Lakini sikuwa na budi kutekeleza majukumu yangu ili kipato kizidi kuongezeka. Tukiwa tunaendeleza huduma zetu kwa wateja, nikapigiwa simu kwa namba ngeni. Hakuwa mwingine bali ni mama mwenye nyumba. "Unaweza kuja hapa Tanzanite hotel muda huu?" ni swali aliloniuliza baada ya salamu. Kuangalia muda ulikuwa muafaka kwa mahanjumati. Kwanini nikatae ofa? Tena ofa katika muda muafaka? Ukizingatia tayari nilishajua nia yake. Alikuwa akitaka kuonja utamu wangu. Lakini ni mke wa mtu. Haijalishi! "Nipe dakika tano nitakuwa hapo" nilimjibu. Sikutaka kumshirikisha Sam jambo hilo, nikamuaga na kuchukua bodaboda kuelekea Tanzanite hotel. Nilipofika nikamkuta mama mwenye nyumba akiwa anaishusha taratibu soda aina ya mountaindew. Akanionyesha uchangamfu wa hali ya juu. "Nilifikiri usingekuja" aliniambia huku akinikazia macho usoni mwangu. "Kwani una nia mbaya na mimi hadi niogope? Labda mzee atukute hapa ndo itakuwa balaa maana atahoji kinachoendelea" nilimwambia wakati huo nilishaletewa ugali samaki niweze kuituliza njaa yangu. "Aah! Kumbe muoga hivyo hee? Ili vizuri uwe muoga lakini hayupo kasafiri na atarudi baada ya wiki moja" alizidi kunimwagia sera utadhani wanasiasa mbele ya hadhara. Taratibu nikiwa naendelea kuyatia tumboni matonge ya ugali, stori za utani zilikuwa zikiendelea utadhani ni watu tulio sawa kwa rika. Kumbe kanizidi miaka kama ishirini. Dakika kadhaa kimya kikatawala baina yetu pale wateja wawili walipokaa jirani yetu. "Kuna kazi nataka nikupe kesho usiku ukitoka kazini." aliuvunja ukimya wale watu walipoondoka na kutuacha sisi tukiburudika kwa vinywaji baridi visivyokuwa na kilevi ndani yake. "Mh! Kazi gani hiyo tena ya usiku? Na ukizingatia nikitoka kazini nakuwa na uchovu? Huoni itakuwa vigumu kuifanya kwa ufasaha japo Mererani kilichonileta ni kutafuta fedha?? "Usitie shaka. Si kazi ngumu lakini utapata malipo mazuri pengine kuliko fedha unayoiingiza kwa wiki moja kazini kwako." "Mimi ni mtafutaji na bado sijapata. Lakini nidokeze ni kazi gani ili nijipe muda wa mapumziko kwa kumuachia kijana wangu kazi leo na kesho." "Haraka iweke pembeni mradi nimeshakwambia ni kazi nyepesi na yenye malipo mazuri" alinijibu kisha akainuka na kwenda kulipia bill yetu. Hapakuwa na lingine zaidi ya kuondoka kila mmoja na njia yake. Nilipofika kazini nikamuomba Sam aendeleze majukumu pamoja na kumtaarifu kwamba kesho yake nisingeripoti kazini. Nashukuru alikuwa muelewa hivyo nikaelekea nyumbani kujipumzisha. Sikuhitaji usumbufu kutoka kwa mtu yeyote, nikazima simu yangu na kujitupa kitandani kama mzigo hata bila ya kuoga. Nikapitiwa na usingizi mzito. Niliposhtuka ilikuwa ni majira ya usiku. Njaa ikiwa kali tumboni mwangu. Nikainuka kiuchovu lengo langu likiwa kwenda kutafuta chakula kwakuwa nilihisi uvivu wa kupika. Lakini nikapigwa na mshangao pale macho yangu yalipotua kwenye meza yangu ndogo iliyokuwa mle chumbani. Hotpot ikiwa juu yake. Haa! Nilistahili kushangaa. Nikapiga hatua na kuisogeleg. UNASTAHILI. Maandishi makubwa kwa rangi ya kijani yalisomeka kwenye karatasi iliyofunika hotpot ile. Ni nani huyu aliyefanya hili? Nilijiuliza. Instagram @kulayasimulizi Nilipaswa kujiuliza juu ya mtu aliyekiweka chakula kile. Ni Edna au? Mke wa mwenye nyumba au? Nilijikuta njia panda ghafla. Lakini njaa inanisulubu kweli. Acha nile. Nikanawa mikono na kukifakamia chakula kile kwa fujo. Ilikuwa ni tambi na nyama. Tena ambazo ni ugonjwa wangu. Zile za kutiwa sukari na siyo za chumvi kama wafanyavyo baadhi yao. Sikubakisha hata kidogo maana utamu wake ulikuwa si mchezo. Nilipomaliza nikamimina maji baridi ya wastani na kushushia. Ewalaa! Mambo si ndo hayo? Nikawa nimeshiba kwa kula chakula nisichojua kitokako. Nikafungulia muziki laini ili kupotezapoteza muda. Nikiwa naburudika kwa burudani hiyo, nikakumbuka kuwasha simu yangu. Hazikupita dakika mbili, meseji tatu zikaingia mfululizo. Ya kwanza ilitoka kwa Emmy. "Mbona unanitesa hivi mwenzio?" Hiyo sikuona umuhimu wake. Nikafungua nyingine. Hiyo ilitoka kwa Nasra. "Unaonaje nifanye mbinu niwezavyo ili kesho tulale wote tukipeana mambo usiku kucha hadi tutosheke?" Hiyo ilinifanya nigune. Kwakuwa kesho ndo nilikuwa na miadi kwa mke wa mwenye nyumba. Nikamjibu kwa kumwambia afanye siku nyingine. Hakuwa mbishi sana. Akanielewa kwa kupanga siku mbili mbele. Iliyofuata ilikuwa ikisomeka hivi, "Umeshiba mawazo yangu?" namba ilikuwa ni ile ngeni iliyonipigia mchana. Haikuwa ya mwingine bali ni ya mke wa mwenye nyumba. Unaweza kuwa umechanganywa na meseji yake hiyo kwa kumaanisha tofauti. Yani mimi kushiba mawazo yake. Utakuwa umekosea. Alichomaanisha ni mimi kuwa sumbuko la fikra zake. Aliniwaza sana. Kwa wapenzi huenda angeniuliza, 'laaziz wangu umeshib?' au angetumia neno lolote linaloashiria mahaba. Ila huyu alikuwa bado. Ndo maana akasema mawazo yake. Loh! Wanawake wengine bhana! Si ana mume wake? Iweje aniwaze mimi badala ya mume wake aliyeko safarini? Nikaamua kumjibu. "Nimeshiba sana mpaka namtamani wa kunipunguza shibe. Lakini umepata wapi ujasiri wa kuingia ndani kwangu? Huoni litakuwa tatizo kama utakuwa umeonekana?" "Ujasiri hauuzwi lakini nashindwa kujizuia" alinijibu na kunifanya nicheke. Aisee! Alikuwa ni mkubwa eti! Sema tu uzuri na umbo lake vilikuwa vikivutia. Changanya na rangi yake maji ya kunde. Kwanini udenda usinitoke hata kama yupo sawa na mama yangu? Si nitakuwa namtendea dhambi shetani kwa kumuacha mama huyu? Eti wasomaji ningekuuliza kipindi hicho ungenishauri nini? Maana huyo mama mvuto wake unakolezwa na hayo macho yake ya mduara. Jamani aah! Wacha nifaidi tu mengine mbele ya safari. "Haya mama" unajua alinijibu nini? Soma tu. "Niite mama mbele za watu lakini tukiwa wenyewe unaruhusiwa kuniita Sabrina" mh! Nilichoka kwa maneno yake. Tulichat kwa muda mrefu na kabla hajanitakia usiku mwema alinisisitizia kujiandaa kwa kazi yake atakayonipa kesho. Muda ulishaenda, nikafunga mlango na kurejea kitandani. Nikiwa usingizini, nilishtuliwa na mlio wa simu yangu. Nilipoangalia mpigaji alikuwa ni Emmy. Saa ilionyesha saa nane usiku. Kulikoni tena? Niliwaza kabla ya kuipokea. Ikaendelea kuita nikiwa naiangalia hadi ilipokata. Dakika kadhaa ukaingia ujumbe mfupi kutoka kwa Emmy uliosomeka hivi, "Natoroka nyumbani nije kwako. Halafu naacha ujumbe wa kuwaelekeza niendako ili nikipata matatizo wajue pa kuanzia. Nimeshindwa kulala Emma kwa ajili yako. Kwanini nipate tabu kiasi hiki wakati tabibu upo?" Nilishtushwa sana na ujumbe ule. Usiku wote ule tena kwa mtoto wa kike si sherehe kwa wahuni? Nilijikuta nikitetemeka na jasho kunitoka kwapani japo haikuwahi kunitokea hapo kabla. Balaa gani tena hili linalotaka kuniharibia maisha? Yani niende jela kisa kitendo cha nusu saa? Nikapata wazo ambalo niliona litaweza kunifaa. Instagram @kulayasimulizi "Nakuahidi keshokutwa nitamaliza tatizo lako. Nakuomba sana Emmy. Na nisipotimiza fanya lolote la kunidhuru." Huuu! Nilishusha pumzi ndefu alipotuliza mzuka wake kwa kunitaka kutoleta masikhara siku niliyomuahidi. Nikarudi usingizini. Yani ile alfajiri kabla ya wale ndugu zangu waislam hawajaadhin, mlango wangu ukagongwa. Nikaamka na kwenda kufungua. Hamali! Mke wa mwenye nyuma kabebelea hotpot. Akanipa na kuniambia maelezo mengine kwenye meseji. Akaondoka na kuniacha nikicheka peke yangu. "Hiyo ni supu. Ukifika muda wako utakaouona unakufaa utapasha unywe halafu upumzike. Leo sitaki upate tabu maana hiyo kazi nnayotaka unifanyie siyo ya kitoto" hayo ndo yalikuwa maelezo ya meseji yake. Kweli ukitaka kuyajua mengi toka kwa walimwengu, kuwa mtembezi. Mazuri kwa mabaya utayajua. Siku hiyo nilishinda ndani kwangu. Muda niliotoka ilikuwa ni kwenda kula chakula cha mchana. Nadhani alishindwa kuniletea kutokana na mazingira kuwa hatarishi mchana ule. Masaa yalienda kasi mno. Ilipotimu majira ya saa mbili usiku, akanitumia meseji. "Fanya haraka. Nazima taa ya nje ili uingie ndani kwangu" huyu mama mtaalamu kweli. Sikuchelewa, nikafunga mlango wangu na bahati nzuri pale nje hapakuwepo mtu. Taa ilipozimwa tu nikawahi chap na kuingia ndani ya nyumba tayari kwa kazi niliyoahidiwa malipo mazuri. Nikajifanya kutofahamu nia yake kwa kumwambia, 'nipatie vifaa vya kazi ili tusipoteze muda' ujue sikuwa nimemuangalia usoni nilipoingia mle ndani. Macho yake sijui alikuwa ameyafanyaje maana yalikuwa kama yanadondoka. Yaani yamelegea hadi huruma ikanikumba. "Nifuate nikuonyeshe kazi yenyewe" aliniambia huku akitembea kuelekea kwenye korido iliyotenganisha vyumba. Hata mwendo wake haukuwa wa kawaida kama nilivyozoea kumuona. Alitembea kwa kujilazimisha. Usipate tabu msomaji wangu kwanini alikumbwa na hali hiyo. KUNGU. Halafu mwanga hafifu wenye rangi ya kijani ndani ya nyumba ile, ulichangia kuyalegeza macho yake. Safari yetu ikaishia chumbani. Chumba kikiwa katika hali ya utulivu na manukato yenye kustarehesha pua za mnusaji. Zulia jekundu na la manyoya likiwa limetandikwa chini huku likipambwa kwa maandishi meupe yaliyosomeka hivi, 'ukipewa kula' nile nini? Chakula hakipo mezani? Oooh! Kumbe chakula chenyewe ni mwili wa mwanamke aliyesimama mbele yangu bila nguo yoyote mwilini mwake. Alishajiandaa kumbe ile khanga iliyouficha mwili wake nilipoingia ndani, haikuwa imefunika nguo yoyote. Hivyo tulivyoingia ndani akaifungua na kuiacha idondoke yenyewe na kumuacha katika hali ya matamanisho mwanaume Emma. Nikiwa katika kuduwaa.. yule mama a…. Whatsapp +255 758 018 597 au Pakua app bofya link HAPA

Post a Comment

0 Comments