Nilikurupuka
usingizini, mapigo ya moyo wangu yalienda kasi sana,ndoto niliyoota ilikuwa ya
kutisha, sikutamani hata kuelezea. Nilinyanyuka kitandani, nikaisogelea swichi,
karibu na mlango, nikawasha taa!
“,Whaaat!
wewe ni nani?, ina maana nilikuwa naota ndoto ya kweli! “,niliongea kwa
mshangao, binadamu wa kutisha, niliyemuota ndotoni akinikimbiza, alikuwa mbele
yangu amesimama,mwanga wa taa kubwa ya umeme ulimfanya aonekane wazi juu mpaka
chini,ngozi yake ilikuwa nyeupe kama karatasi,mdomoni alifungwa kitambaa
cheupe, kichwani alikuwa na michirizi ya damu.
“,Nimekuja
nimekuja nimekuja, nimekuja kuitoa roho yako! “,binadamu yule wa kutisha
aliongea, akipiga hatua kunisogelea,ilibidi nifanye kila njia kuiokoa nafsi
yangu, nikataka kukimbia, sikuweza, mlango wangu niliufunga kwa funguo kabla ya
kulala, isitoshe funguo zilikuwa kitandani, nisingeweza kuzifuata, binadamu
yule angenikamata kwa urahisi, aliendelea kutembea taratibu kama roboti
kunisogelea, hakutembea kama binadamu wa kawaida, alitembea kwa kujiburuza
sakafuni.
“,Mungu
wangu, nimekwisha! “,nilitamani ardhi ipasuke niweze kutoka,haikuwezekana.
“,Wewee…e
ni nani?, unataka nini kw…angu ……?”,niliuliza huku nikitetemeka,kwa mara ya
kwanza nilijikojolea, niliumbuka mwezenu.
“,Naitwaa
Tagrisi, mfalme wa ujinini, umenikosea sana, umenikosea, umenikosea, nimekuja
kukuua, kukuua! “,nilizidi kuchanganyikiwa,nikalitazama juu mpaka chini, kweli
alikuwa jini, alikuwa na kwato nyeusi, nguvu zikaniishia, nikatafakari kosa
nililolifanya, sikupata jibu,kwa mbali macho yangu yakaona giza, nikahisi
kizunguzungu, nikazimia palepale na kudondoka chini.
…………………………………
02:20pm
Baada ya kuzimia, jini lile lilitoweka,lilitaka kuniuwa
mpaka nitakapotambua makosa yangu,makosa ambayo sikuyafahamu. Ghafla fahamu
zikanirejea tena, nilikuwa nahema na kupumua kwa kasi, mapigo yangu ya moyo
hayakuwa ya kawaida,nikatazamaa juu ya dali sikuona kitu, kulia na kushoto,
sikuona kitu, nikatazama chini ya uvungu, sikuona kitu chochote kile,
nikaisogelea friji yangu, nikamimina maji kwenye glasi, nikanywa,angalau mwili
wangu ukapoa, joto likapungua. Taratibu nikakisogelea kitanda changu, nikalala
tena, baada ya dakika tano tu, usingizi mzito ukanichukuwa, nikaanza kuota
ndoto nyingine ya kutisha, niliota nikiwa katikati ya msitu, mikono na miguu
yangu ilifungwa kwa kamba ngumu ya katani. Jini yule aliyejitambulisha kwa jina
la Tagrisi, alikuwa ameshika panga,nyuma yake alikuwa na wafuasi wake,
walifanana kwa kila kitu, mavazi yao ya rangi nyeusi, ngozi nyeupe pamoja na
michirizi ya damu kichwani.
“,Umenikosea
sana, umenikosea sana, lazima ufe, lazima ufe, lazima nyama yako niwapatiee
wafuasi wangu, wafuasi wangu ……”,jini aliyejitambulisha mbele yangu kwa jina la
Tagrisi aliongea, akanyenyua panga lake kubwa, lililong’aa kutokana na makali
yake, alitaka kuninyofoa kiungo kimoja baada ya kingine,akalishusha panga lake
kwa kasi ya ajabu aweze kuifyeka shingo yangu…“,Mamaaaa, nakufaaaa!” Tukutane
Whatsapp +255 758 018 597
Nilikurupuka
usingizini, mapigo ya moyo wangu yalienda kasi sana,ndoto niliyoota ilikuwa ya
kutisha, sikutamani hata kuelezea. Nilinyanyuka kitandani, nikaisogelea swichi,
karibu na mlango, nikawasha taa!
“,Whaaat!
wewe ni nani?, ina maana nilikuwa naota ndoto ya kweli! “,niliongea kwa
mshangao, binadamu wa kutisha, niliyemuota ndotoni akinikimbiza, alikuwa mbele
yangu amesimama,mwanga wa taa kubwa ya umeme ulimfanya aonekane wazi juu mpaka
chini,ngozi yake ilikuwa nyeupe kama karatasi,mdomoni alifungwa kitambaa
cheupe, kichwani alikuwa na michirizi ya damu.
“,Nimekuja
nimekuja nimekuja, nimekuja kuitoa roho yako! “,binadamu yule wa kutisha
aliongea, akipiga hatua kunisogelea,ilibidi nifanye kila njia kuiokoa nafsi
yangu, nikataka kukimbia, sikuweza, mlango wangu niliufunga kwa funguo kabla ya
kulala, isitoshe funguo zilikuwa kitandani, nisingeweza kuzifuata, binadamu
yule angenikamata kwa urahisi, aliendelea kutembea taratibu kama roboti
kunisogelea, hakutembea kama binadamu wa kawaida, alitembea kwa kujiburuza
sakafuni.
“,Mungu
wangu, nimekwisha! “,nilitamani ardhi ipasuke niweze kutoka,haikuwezekana.
“,Wewee…e
ni nani?, unataka nini kw…angu ……?”,niliuliza huku nikitetemeka,kwa mara ya
kwanza nilijikojolea, niliumbuka mwezenu.
“,Naitwaa
Tagrisi, mfalme wa ujinini, umenikosea sana, umenikosea, umenikosea, nimekuja
kukuua, kukuua! “,nilizidi kuchanganyikiwa,nikalitazama juu mpaka chini, kweli
alikuwa jini, alikuwa na kwato nyeusi, nguvu zikaniishia, nikatafakari kosa
nililolifanya, sikupata jibu,kwa mbali macho yangu yakaona giza, nikahisi
kizunguzungu, nikazimia palepale na kudondoka chini.
…………………………………
02:20pm
Baada ya kuzimia, jini lile lilitoweka,lilitaka kuniuwa
mpaka nitakapotambua makosa yangu,makosa ambayo sikuyafahamu. Ghafla fahamu
zikanirejea tena, nilikuwa nahema na kupumua kwa kasi, mapigo yangu ya moyo
hayakuwa ya kawaida,nikatazamaa juu ya dali sikuona kitu, kulia na kushoto,
sikuona kitu, nikatazama chini ya uvungu, sikuona kitu chochote kile,
nikaisogelea friji yangu, nikamimina maji kwenye glasi, nikanywa,angalau mwili
wangu ukapoa, joto likapungua. Taratibu nikakisogelea kitanda changu, nikalala
tena, baada ya dakika tano tu, usingizi mzito ukanichukuwa, nikaanza kuota
ndoto nyingine ya kutisha, niliota nikiwa katikati ya msitu, mikono na miguu
yangu ilifungwa kwa kamba ngumu ya katani. Jini yule aliyejitambulisha kwa jina
la Tagrisi, alikuwa ameshika panga,nyuma yake alikuwa na wafuasi wake,
walifanana kwa kila kitu, mavazi yao ya rangi nyeusi, ngozi nyeupe pamoja na
michirizi ya damu kichwani.
“,Umenikosea
sana, umenikosea sana, lazima ufe, lazima ufe, lazima nyama yako niwapatiee
wafuasi wangu, wafuasi wangu ……”,jini aliyejitambulisha mbele yangu kwa jina la
Tagrisi aliongea, akanyenyua panga lake kubwa, lililong’aa kutokana na makali
yake, alitaka kuninyofoa kiungo kimoja baada ya kingine,akalishusha panga lake
kwa kasi ya ajabu aweze kuifyeka shingo yangu…“,Mamaaaa, nakufaaaa!” Tukutane
Whatsapp +255 758 018 597
0 Comments
Karibu sana, tuma ujumbe whatsapp +255 758 018 597 kujipatia simulizi zetu
Emoji