Tegemeo hasi (Riwaya) - Utamu 18+




“sasa amepita hapa akaona anisalimie kidogo mzee wake,” alijibu mzee Hewa... “Ahaa! Oke...halafu anaondoka zake?” baba Mei alitaka kujua zaidi... “Anaondoka...kwani vipi?” “Nimeuliza tu mzee wangu...” “Ataondoka...ataondoka.” Baba Mei alirudi kwanza ndani kisha baada ya kama dakika tano akatoka huku akisikika akisema... “Ole...ndiyo utanitambua mimi nani?!” Baada ya baba Mei kuondoka, mzee Hewa na Jombi walijadili lile swali... “Huyu bwana inaonekana amekutilia wasiwasi...maana kijana kama wewe kuja hapa
na mke mwenyewe kama huyu ni tatizo,” alisema mzee Hewa... “Hata mimi nimemshangaa hivyohivyo mzee Hewa kwani asingeweza kusema maneno yale mbele yangu huku nasikia...afadhali angekuuliza nikiwa sipo,” alisema Jombi huku moyoni yeye akiijua dhamira iliyompeleka pale... “Jana nilisoma gazeti moja linasema hizi nyumba zetu hapa zitabomolewa, we unazo habari hizi?” mzee Hewa alikata maongezi ya awali na kumuuliza Jombi hivyo... “Hapana mzee Hewa, ni kweli?” “Ngoja nikalilete na wewe upitie habari hizo,” alisema mzee Hewa huku akisimama kwenda ndani akiimba nyimbo za dini kama ilivyo kawaida yake. Mara, mama Mei alitoka. Safari hii alikuwa amejifunga kitenge, mkononi alishika kipochi kidogo, ilionekana alikuwa akienda dukani au gengeni. Licha ya kuvaa kitenge ambacho kilikaribia kuburuza chini lakini mzigo ulionekana kama kawa... “Anti naona unafuata bidhaa dukani sasa!” alisema Jombi. Mama Mei alimwangalia
kwa jicho la uchokozi kisha akasema... “Ni kweli lakini leo jua kali kama nini Mungu wangu, sijui niende na mwamvuli...” “Hata mimi nashauri hivyo maana...au nitume mimi.” Mama Mei alicheka huku akimkazia macho Jombi... “Yaani nikutume wewe anko si itakuwa dharau kubwa... nakwenda pale buchani na kwenye lile soko la pale kona...” “Nitume tu anti,” Jombi aling’ang’ania kutumwa. “Kweli?” mama Mei alitaka kujua ya moyoni... “Kweli kabisa anti,” alisema Jombi huku akisimama tayari kwa kutumwa... “Basi asante, nataka nyama kilo tano maana huwa naiweka kwenye friji kwa wiki nzima. Halafu nataka kabeji tatu... nazi sita...viazi mviringo kisado na mchele kilo tano,” alisema mama Mei... “Mh!” Jombi aliguna moyoni baada ya kupata picha ya ukubwa wa mzigo atakaobeba. *** Jombi, licha ya kufanya kazi serikalini tena ya maana, pia ni mume wa mtu, bidhaa alizojituma kununua na maeneo zinakopatikana na nyumbani kwake ni jirani tu,
hivyo alikwenda kwa mahesabu sana. Alipokuwa kwenye soko alikumbana na maneno haya... “Baba Hawa leo umekuja mwenyewe? Mama vipi..?” “
Leo baba Hawa nakuona umeamua kufuatilia mahesabu mwenyewe.” Mpaka mwisho anaondoka akiwa amebeba mfuko mkubwa kabisa, hivyo aliamua kuchukua Bajaj japokuwa alikokuwa anakwenda si mbali sana. * Mzee Hewa alishangaa kukuta Jombi hayupo nje alikomwacha... “Kha! Huyu bwana vipi tena?” alijiuliza bila kupata majibu kwani hakumkuta mama Mei, aliingia ndani akijua anko huyo akirudi na mizigo atamwita. * “Baba Hawa hiyo mizigo unaipeleka wapi mume wangu? Sikuelewi,” sauti ya mkewe, mama Hawa ilimshtua kwa nyuma akiwa anapanda Bajaj...
“Ohoo! Ni mzigo wa baba Kabweka, kaniambia aliacha hapo sokoni, sasa kwa vile mimi nakwenda kule kwake kaomba nimbebee,” alipiga uongo Jombi... “Sawa mume wangu.” Jombi alipona, alipeleka mizigo hiyo hadi nyumbani kwa mzee Hewa na kukutana na mzee huyo nje. Alishangaa kumwona Jombi anaingia na Bajaj tena na mizogo wakati dakika chache nyuma, alikaa naye hapo... “Imekuaje tena kijana wangu? Mbona natoka na gazeti sikuoni?” Huyo dada mpangaji wako aliniagiza sokoni.”
Mara, mama Mei mwenyewe alitokea huku akimshukuru sana Jombi... “Jamani anko yaani sijui nikupe zawadi gani? Yaani nashukuru kama nini...yaani eee...na jua hili nilikuwa najifikiria sana yaani...” alisema mama Mei huku akijifunga kanga vizuri kwani alitoka na kanga moja tu... “Si unipe mimi mwenyewe nafasi ya kuchagua zawadi anti,” Jombi alijisemea moyoni...Usijali anti...sisi ni wamoja mbona,” alisema Jombi. Baada ya Bajaj kuondoka na mama Mei kuzama ndani na mizigo yake, mzee Hewa alimtupia jicho Jombi... “Kijana,” aliita... “Naam...” “Kuna kitu...” “Kuhusu nini mzee Hewa..?” “Huyu mama wewe unajuana naye?” “Wala! Ametoka tu hapa akasema anasikia jua kwenda kununua vyakula nikamwambia lete hela nikakununulie.”
“Basi, umejishindia kijana wangu....maana kama ni mke wa mtu na anajitambua halafu anafikia hatua ya kukuamini wewe kijana mkubwa ukamfanyie manunuzi, mshukuru Mungu maana wenzako wengi wanapitapita hapa kila siku kufukuzia,” alisema mzee Hewa. Moyoni, Jombi aliamini yeye ni mshindi kama kweli kuna wenzake wanapitapita kufukuzia halafu yeye kafikia levo ile, basi yupo juu... “Yes! Mshindi mimi bwana,” alisema moyoni Jombi... “Hapana mzee Hewa mimi binafsi sina lengo baya na mke wa mtu...kwanza mimi ni muoga sana na wake za watu,” alisema Jombi huku akilichukua gazeti kwa mzee Hewa na kusoma habari aliyoambiwa. Mama Mei akatoka tena, safari hii alikata kona kwenda kwenye kiduka cha jirani. Alikuwa ndani ya kanga moja tu, sasa ile tembea yake na mtingishiko wa wowowo, mzee Hewa alijishika kichwa licha ya umri wake mkubwa, Jombi yeye alijiinamia.
Walinyamza kimya! Kimya kabisa!! Wakati anarudi sasa, macho yake yalikutana na macho ya Jombi yakiwa yameoneka kuumizwa, mama Mei akaachia tabasamu pana kwa maana ya kuweka ukaribu wa kibinadamu kwa vile alimsaidia jukumu la kununua mahitaji. Jombi naye aliachia tabasamu la woga, akamwangalia kwa kumsoma kuanzia juu kwenda chini, mama Mei akazama ndani kwake. Safari hii, mpaka Jombi anaondoka zake, mama Mei hakuwa ametoka tena. Mbaya zaidi, hatua chache mbele, Jombi alipishana na mume wa mama Mei akiwa anarejea nyumbani kwake. Walikutana macho, baba Mei alionekana kummaindi sana Jombi. *** Siku ya tatu, jioni, Jombi alishatoka kazini sasa alikuwa akirandaranda mitaani, akaibukia mtaa wa jirani na kwa mzee Hewa ambapo pana baa.
Alikaa hapo. Katika kutupia macho, akamwona mama Mei amekaa sambamba na mume wake, alishtuka... “Ohoo! Jamaa si atajua namfukuzia mke wake, maana nabanana naye sana,” aliwaza moyoni. Mama Mei naye, katika kupitishapitisha macho, akamwona Jombi, akafurahia moyoni kwani alikumbuka alivyomtuma sokoni... “Wanaume wengine jamani, wakarimu kweli. Baba Mei umtume vile sokoni, mbona atakung’oa meno,” alisema moyoni mama Mei. Kuna wakati baba Mei alikwenda chooni, mama Mei akatumia nafasi hiyo kulisisitiza jicho lake kwa Jombi ambapo yalikutana, mama Mei akaachia tabasamu na kupunga mkono, Jombi naye akapunga mkono, wakaachiana tabasamu.
Baba Mei alipotoka chooni, hakukaa, aliondoka na mkewe huku baa yote wakimtupia macho, wake kwa waume. Baadhi yao walionesha kutingisha vichwa vyao kutokana na umbo la mama Mei. Jioni hiyo, alivaa suruali ya kubana na t-shirt pia ya kubana, sasa wakati anakanyaga chini ili mguu uende mbele, looo! Wanaume walionekana kuumia ndani kwa ndani, wengine walisemezana kwenye meza. Kwa upande wake, Jombi alionekana kuumia zaidi kwani alimkodolea macho mwanamke huyo mpaka anapotea na mume wake huku moyoni akiumia kama vile mwanamke alikuwa wake sasa ameporwa na mwanaume mwenye fedha zake.
Saa mbili usiku, Jombi aliondoka kwenye baa hiyo kurudi kwake, lakini akaamua kupitia njia ya kwa mzee Hewa akiamini anaweza hata kusikia sauti ya mama Mei... “Yule saa hizi atakuwa ameshalala,” alisema moyoni Jombi. Alipita nje ya nyumba hiyo huku macho na masikio yakiwa hapo. Ghafla alisikia mlango mkubwa ukifunguliwa kwamba kuna mtu anatoka. Jombi alisimama na kukazia macho mlangoni, moyoni alimwomba shetani wake amsaidie kwamba, anayetoka awe mama Mei... “Yaani akinipa dakika tatu tu ya kunisikiliza atajua mimi ni nani na naamini ataingia laini,” alisema moyoni Jombi huku macho yake yakitamani sana kumwona anayetoka.
MWANAUME mmoja mnene, mrefu, mweusi tii ndiye aliyetoka akiwa amevaa singlendi kwa juu, chini pensi. Alionekana ana asili ya ukorofi... “Mbona umesimama hapo kijana, una shida na nani?” aliuliza yule mwanaume huku akikohoa. “Hapana, napita tu,” Jombi alijibu kwa upole huku akianza kutembea. Lakini muda huohuo, mama Mei alichomoza kwenye mlango mkubwa, akashuka ngazi na kuelekea uelekeo wa ile baa waliyokaa. Kwa usiku ule na kwa kutumia mwanga wa taa ukijumlisha na tembea yake, hata yule mwanaume pale nje alimwangalia kwa macho yenye matamanio makubwa...
“Haya bwana, ulimwengu shujaa,” alisema yule mwanaume huku mama Mei kama vile anafanya kusudi sasa, maana ungeweza kusema mzigo utaanguka wakati wowote ule. Jombi alitamani kugeuza njia kwani aliamini mama Mei anarudi kule baa kwa ajili yake. Alichofanya, alikatiza mbele akageuza kwa njia nyingine na kutokea baa. Alivuta kiti na kukaa huku macho yake yakimulika kila kona kama atamwona mama Mei. Lakini hakumwona! Jombi alijisikia unyonge sana, akaondoka kurudi kwake lakini safari hii akitumia njia nyingine. *** Ilikuwa siku iliyofuata asubuhi, mzee Hewa alikuwa uani akipiga mswaki ili afuate mafao yake, NSSF, mama Mei alitoka ndani kwake akiwa ndani ya kanga moja tu... “Shikamoo mzee Hewa...” “Marahaba mwanangu, umeamkaje mama?” aliitika mzee huyo huku akimwangalia mama Mei anavyokwenda chooni huku wowowo likisomeka kwa baba mwenye nyumba wake
kwa mtetemeko... “Leo mbona asubuhi sana mzee Hewa?” mama Mei alimuuliza bila kusimama... “Nafuata vijisenti vyangu NSSF bwana...” “Ahaa! Kavilite tule hata nyama,” mama Mei alimtania mzee huyo. Mzee Hewa hakuongeza neno kwani tayari mama Mei alishazama chooni åΩLakini wakati anatoka, baba Mei naye alikuwa ameshatoka alikuwa uani hapo akipiga mswaki. Kwa hiyo mzee Hewa alishindwa kutia neno mbele ya mali za watu... “Hivi wewe mbona hunisikii?” baba Mei alimuuliza mkewe kwa sauti ya chini lakini yenye hasira sana, mama Mei hakujibu, akaenda ndani. Kwa mzee Hewa baba Mei kumlalamikia mkewe kwamba hamsikii ilikuwa kama mara ya saba tangu wamehamia pale... “Kama ni mara saba je mara ambazo mimi sijasikia ni ngapi? Kuna jambo, huyu mama hataki kumsikia mume wake na hawa ndiyo wanawake wetu siku hizi,” alisema moyoni mzee huyo, akaenda kuoga akarudi
ndani kwake kujiandaa. Baba Mei ndiye aliyeanza kutoka ndani ya nyumba ile. Wakati mzee Hewa anatoka, alimwita ili ampe lifti... “Ameshaondoka mbona,” alijibu mama Mei... “Ooo! We upo?” mzee Hewa alimuuliza akiwa amesimama mlangoni, mama Mei akatoka huku na kusimama mlangoni... “Mimi nipo baba,” alisema mama Mei. Mzee Hewa alimwangalia mama Mei, mama Mei naye akagundua anamwangalia, wakaangaliana, mama Mei akainamisha uso... “Hivi mjukuu wangu...” “Abee...” “Mumeo anapenda kukulalamikia kwamba humsikii, kuna nini kati yenu?” Mama Mei akaachia tabasamu... “Mzee Hewa, baba Mei hana lingine zaidi ya wivu. Yeye hataki mimi nivae kanga, nivae suruali, anataka nivae magauni makubwa tu...sasa kwa mfano saa zile natoka kwenda chooni, nivae gauni kama nakwenda kanisani, inawezekana kweli..?
“Haya, kama vile haitoshi, hali ya jiji letu la Dar inafahamika, sasa mchana na jua kali mimi naenda sokoni, nivae gauni kama nakwenda kwenye mkutano wa wazazi shuleni, ni sawa kweli?” Mzee Hewa alibaki akisikiliza, ikafika mahali akasema... “Kuna dozi yake nitakupa...” “Ya kunywa ya kumeza?” aliuliza kwa haraka mama Mei... “Ya kawaida tu, wivu wote huo utakwisha...” “Kweli mzee Hewa? Maana ananikwaza sana ujue...” “Dawa yake ndogo tu nitakupa dozi mimi,” alisema mzee huyo huku akiondoka... “Mzee Hewa naisubiri kwa hamu kubwa hiyo dozi,” mama Mei alimsindikiza kwa maneno hayo. *** Alasiri ya saa tisa, mzee Hewa alirudi kabla baba Mei hajarudi, alimkuta mama Mei amekaa nje kwenye mkeka.
“Pole mzee Hewa, inabidi uoe sasa...maana kama hivi umerudi huna wa kukupikia,” alisema mama Mei kwa sauti iliyojaa utani... “Kama wewe upo mimi sina haja ya kuoa,” mzee Hewa naye alirudisha utani... “Wee! Unataka kupigwa mzee Hewa? Hivi hapa nilikuwa nakusubiri kwa hamu kubwa unipe hiyo dozi uliyoahidi,” alisema mama Mei...
“Njoo ndani nikupe dozi yake,” mzee Hewa alisema akiingia. Mama Mei alisimama, akamfuata mzee huyo kwani ni kweli kutoka moyoni alitamani sana kupata ufumbuzi juu ya wivu mkubwa alionao mume wake, baba Mei. Mzee Hewa alizama hadi chumbani, mama Mei yeye akasimama akijua mzee huyo atatoka... “Pitapita mama Mei pita,” alisema mzee Hewa huku akiangalia mlangoni. Hapo alikuwa sebuleni kwake, sebule ambayo ilisheheni vitu vya kisasi licha ya uzee wake... “He! Mzee Hewa, mpaka niingie ndani jamani?” aliuliza mama Mei huku akifungua mlango. Mzee Hewa alisimama, akafunga mlango na funguo kisha akazichomoa...
Kama kawaida ni
Whatsapp +255 758 018 597
Email – emanmic@yahoo.com


Post a Comment

0 Comments