Sikutegemea mama (Riwaya) - Utamu




Jastin ni kijana mwenye miaka ishirini, nimpole sana kumsikia anaongea ninadla sana, hata uongeaji wake niwataratibu sana, tena uongea mara chache na kwa sauti ya chini, hata huko shuleni alikokuwa anasoma wenzake walikuwa wanamwita paroko.
Kwa sasa Jastin alikuwa amemaliza kidato cha sita, katika shule ya sekondari ya Luhuwiko huko mkoani Ruvuma, kipindi cha kusubiri matokeo alienda Dar es Salaam, kumtembelea kaka yake mkubwa Higno, ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye kampuni moja yausafirishaji, kama dereva wa magari makubwa yamizigo yanayo safari kwenda mikoani na nje ya nchi kupeleka mizigo mbalimbali, kipindi Jastin anafika Dar es Salaam shemeji yake yaani mke wa kaka yake alikuwa ameenda kwao Morogoro kujitazamia kwaajili yakujifungua yaani alikuwa mjamzito, Higno alikuwa anakaa Dar es Salaam mbezi, mtaa wa makondeko, unaingia ndani kidogo ukiihacha barabara kuu iendayo Morogoro, nje kidogo ya jiji Higno alipata eneo dogo nakujenga chumba kimoja na sebule, mtaa huo ulikuwa ni mtaa mpya wenye nyumba chache tu kubwa sana zenye fensi na mageti makubwa na nyumba ndogo kama ya Higno kaka yake Jastin, nyumba za mtaa huu mpya zilikuwa zimeachiana nafasi, kubwa kati ya nyumba na nyumba.
Shuguli za Jastin kila siku, tokea ameingia Dar ni kuweka mazingila safi nakujipikia, kisha anachukuwa simu yake nakufungua facebook hapo ushinda mpaka anaingia kulala, siku moja moja alikuwa akienda na kaka yake ofisini kwao Mwenge huko alimsaidia kaka yake shuguli za ufundi wa gari analo tumia kwa safari za kupeleka mizigo mikoani na nje ya nchi, kama service za kawaida za gari, maana alikuwa anafahamu ufundi wa magari kutokana na baba yao kumiliki garage japo siyo kubwa huko Nachingwea Lindi, lakini kwa Nachingwea magari mengi sana yanatengenezwa pale, ndipo yeye utumia kipindi cha likizo kusaidia kazi ndogondogo za kiufundi.
Siku moja Higno alisafiri kwenda nchini congo DRC, akipitia Rwanda kupeleka magari ya umoja wa mataifa angetumia wiki mbili kwenda na kurudi huku nyuma Jastin alibaki peke yake haikuwa tatizo kwake, siku ya pili toka kaka yake asafiri Jastin aliamka mapema sana akiwa amevalia tracksuit nyepesi, akaanza kufanya shuguli zake za kila siku ikiwa pamoja na mazoezi ya viungo kidogo, tena ufanyia ndani kwao kisha akatoka nje akawasha jiko la mkaa kwa ajili ya kutengeneza kifungua kinywa.
Wakati jiko linakolea akaanza kufagia, wakati anaendelea kufagia akaona geti la nyumba ya jirani yao linafunguliwa, mfunguwaji alikuwa mama mmoja alievalia gauni fupi kidogo lililokamata mwili wake vyema kiasi kwamba Jastin aliweza kushuhudia umbile zuri la yule mama yaani vizuri kabisa, kiukweli hakuwahi kumuona yule mmama zaidi ya binti mmoja ambaye kama siku mbili sasa hajamwona, wakati akiendelea kumwangalia yule mama akamwona amefungua geti kisha akarudi ndani hakuweza kumwona tena sababu ya ukuta mkubwa ulioizunguka ile nyumba mara akasikia mlio wa gari likitoka kwenye lile geti, ni prado nyeusi, likasimama nje kisha akashuka yule mama akaenda kufunga geti, wakati anafunga geti gari likajizima, yule mama alipomaliza kufunga geti alirudi kwenye gari nakujaribu kuliwasha tena lakini alikuwaka, alijaribu mara tatu zaidi alikuwaka akamwona akishuka na kutazama huku na huko, alipotazama upande aliopo Jastin, Jastin akajifanya anaendelea kufagia lakini aliendelea kumtazama kwa macho ya wizi.
“We! anko, We! anko unayefagia” yule mama akaita huku akitazama kule alipo yeye, Jastin akasimama na kujionyeshea kifuani kwamba “Unaniita mimi?” “Ndiyo anko, samahani nakuomba mara moja” Jastin akaweka mfagio chini kisha kamfuata yule mama huku akiuangalia ule mwili wakipekee wa yule mama wa jirani, kila alipozidi kumsogelea ndipo alipoanza kugundua kuwa, licha ya umbile lenye kutamanisha pia huyu mama alijaliwa sura nzuri na ya kuvutia “Shikamoo mama” Jastin alimsalimia yule mmama wa jirani baada tu yakumfikia “Marahaba mwanangu, samahani kwa kukukatisha shuguli zako” aliongea yule mama huku akionyesha uso wa tabasamu, nakufanya midomo yake yenye lips pana zilizopakwa rangi nyekundu ya midomo kumchanganya Jastin japo kwa umri huyu mama ni ni mkubwa sana kwake lakini alionekana bado wamoto “Usijali mama” alijibu Jastin kwa sauti yake ya upole huku akijitaidi kuyakwepa macho mazuri yaliyo kolea wanja ya yule mama, “Wewe ni ndugu wa yule kaka anaekaa pale?” aliongea yule mama huku akionyesha kwa kidole nyumbani kwa akina Jastin, hapo Jastin alipata nafasi ya kushuhudia pete na bagili za dhahabu zilizo jaa mkononi kwa mama huyu, “Ndiyo ni kaka yangu mimi ni mdogo wake wa mwisho” alijibu kwa sauti yake ya upole “Ok! naliacha hapa nje gari langu naomba uniangalizie, maana limezima ghafla” aliongea yule mama akionyesha kupendezwa na upole wa Jastin “Kwani lina tatizo gani?” aliuliza Jastin kwa sauti ileile ya upole, akiligeukia gari la mama wa jirani “Kwakweli mimi hata sijui, yani limezima lenyewe ghafla, nitachukuwa gari jingine hili nalihacha hapa” hapo Jastin akazunguka kwenye boneti “Hebu fungua boneti niangalie kama litawaka” hapo mama jirani akashangaa kidogo, “He! kumbe wewe ni fundi?” aliongea yule mama huku anafungua mlango wa gari kisha akalifyetua boneti “Hapana nina ufahamu mdogo tu wa magari” Jastin aliinua boneti alafu akalizuwia na kifimbo chake cha chuma kisha akaanza kukagua huku akirekebisha kila alipoona panafaa kurekebishwa, lakini kwa macho ya wizi hakuacha kutazama maumbile ya mama jirani yalivyo jichora kwenye kile kigauni matata.
 Whatsapp +255 758 018 597 Kupata Full
Email - emanmic@yahoo.com

Post a Comment

0 Comments