Pambano la Huba (Riwaya) - Kivita, Mapenzi, Kijasusi



Mvua ilikuwa inanyesha sana. Hali ya hewa ilikuwa baridi ikiambatana na upepo wa wastani. Watu wengi hawakwenda kazini, na hata wanafunzi pia wakitega shule kwa kisingizio cha barabara kufurika maji.
Pengine watu hawa walikuwa na hoja kutokana na miundombinu dhaifu ya jiji la Dar es Salaam ambayo haiwezi kurandana na mikikimikiki ya mvua. Ila kwa mwanaume Jonathan Mchau, hilo halikuwa na mashiko kamili kwani yeye alikuwa ofisini akiendelea na kazi zake kama ilivyo ada.
.
Ni ndani ya chumba kidogo kinachopatikana maeneo ya mwenge. Kwenye kuta za chumba hicho kulikuwa kumetundikwa picha kadhaa za kuchorwa kwa mikono. Picha hizi zilikuwa zimeundwa kimafumbo lakini pia zikibeba utajiri wa tamaduni za Afrika kwa ujumla.
.
Kama ungelipata nafasi ya kutembelea hapo basi ungepatwa na kamshangao kidogo kutazama picha hizo zilizofumwa na rangi mbalimbali za kuvutia kiasi kwamba ukasahau kuwa eneo hilo limepakana na barabara yenye makelele lukuki ya magari. Na hata kuta za jengo hilo zina nyufa kadhaa.
.
Mwanaume huyu ajulikanaye kwa jina la Jonathan, Joh, ama Jona kama wamuitavyo watu wa karibu, alikuwa ni mwanaume mweusi mtulivu mwenye mwili wa kujaa, macho makubwa mabovu yasaidiwayo na vioo vya miwani, nywele ndefu kichwani na ndevu alizozichonga umbo la 'o'.
.
Hakuwa mtanashati sana, pengine kwasababu alikuwa kazini na kazi yake aihitaji unadhifu wa hali juu ilhali unacheza na rangi. Ila alikuwa mtulivu sana, na macho yake yaliganda kwenye karatasi aichorayo kwa umakini wa hali ya juu.
.
Alikuwa ndani ya ulimwengu wa peke yake asijali kabisa yanayoendelea nje ya karatasi. Unaweza kudhani mwanaume huyu hakuwa anajua kama kuna mvua ilikuwa inanyesha. Umaanani huu kupita kiasi ukamfanya asifahamu kama kuna mgeni ameingia eneo lake na kusimama kwa sekunde kadhaa.
.
Akashtuliwa, "Hello!"
.
Akatazama na kumkuta mwanamke fulani mrembo, mrefu mwenye rangi maji ya kunde. Alikuwa amevalia sweta rangi ya kijivu iliyofunika blauzi yake nyeupe, pamoja na suruali ya jeans iliyobana vema umbo lake la figa. Miguuni alivalia raba nyekundu.
.
Nywele na masikio yake alikuwa ameyaziba kwa kofia kubwa jeusi la soksi. Mgongoni alikuwa amebebelea begi kubwa jeusi, haya ya kuhifadhia tarakilishi mpakato. Uso wake ulikuwa mfupi na mpole. Macho yake yalikuwa ya wastani ila makali. Mdomo wake mdogo alioupaka rangi ya kahawia ulichanua kwa tabasamu.
.
"Samahani kwa kukutoa kazini," akasema mwanamke kwa sauti ya kumlaghai nyoka.

"Usijali," akadakia Jonathan, "karibu sana." Akaacha kazi akasimama kumlaki mgeni.
"Ahsante. Hapa ndiyo kwa Joh?"
"Yes, ndiyo hapa."
"Na wewe ndiye Joh mwenyewe?"
"Ndio, ni mimi."
"Ook, nimeagizwa na Beatrice Shauri kuulizia mzigo wake."
"Bite?"
"Ndio!"
.
Jonathan akatabasamu. Akafuata mfuko mmoja mkubwa mweupe wa rambo, ndani yake ulikuwa na kitu cha umbo la mstatili, akaunyanyua na kumkabidhi mgeni.
.
"Unaweza ukatazama."
Mgeni akatazama mzigo huo kisha akaurudisha ndani ya mfuko.
"Ahsante sana. Unamdai?"
"Hapana."
"So naweza nikaondoka nao?"
"Hapana." Jonathan akatikisa kichwa. "Siwezi nikakupatia maana sijapata ridhaa ya mmiliki."
"Bite ni dada yangu."
"Taarifa hiyo haijitoshelezi kukupa mzigo wake, dada. Hakunipa agizo hilo."
.
Mwanamke yule akaguna na kubinua mdomo. Akapandisha mabega na kuzungusha macho.
.
"Ok," akasema kwa kupitia puani kisha akaenda zake. Ila punde anarejea tena.
"Kaka mbona unakuwa si mwelewa lakini?" Alilalama. Macho yake yalikuwa yamelegea, mdomo wake ukitepeta.
"Nimekwambia Bite ni dada yangu, ameniagiza. Simu yangu imezima chaji unajua umeme unavyosumbua siku hizi, ningempigia uongee naye!"
.
Joh alipigwa na bumbuwazi. Kuna kitu alikikokotoa kichwani.
.
"Dada," akaita. "Siwezi nikakupa kazi ya mtu. Na hii ni kwasababu sikupewa agizo hilo. Ni swala la uaminifu tu. Sikufahamu, siwezi kukuamini namna hiyo."
.
"Basi ntakuongezea pesa mara mbili ya aliyokulipa Bite," akasema mwanamke huyo kwa kujiamini. Hapo sasa ndiyo Jonathan akapata wasiwasi zaidi. Kwanini mwanamke huyu anataka mzigo huu kiasi hiki?
.
Aliona haja kubwa ya mwanamke huyo ndani ya macho yake. Alikuwa anataka ule mzigo kwa hali na mali.
"Sema basi," mwanamke akasisitiza. Uso wake ulikuwa umekunjana. Alitazama majira ya saa yake kana kwamba mwanafunzi aliyechelewa zamu ya mwalimu mnoko.
"Unataka shilingi ngapi?" Akauliza.
"Sitaki pesa yako," Jonathan akajibu na kuongezea: "Naomba uende, dada."
.
Mwanamke akashusha pumzi ndefu. Akavua begi lake na kuzamisha mkono wake wa kuume ndani. Jonathan akapata shaka. Alitazama mkono huo vema. Alidhani huenda ukatoa silaha.
.
Kabla mkono huo haujatoka ndani ya begi, sauti ya wanaume ikasikika. Jonathan na mgeni wake wakatazama sauti hiyo inapotokea. Mlangoni wakawaona wanaume wawili waliovalia makoti marefu meusi ya kuwakinga na mvua.
.
Wanaume hawa walikuwa warefu na weusi. Mmoja alikuwa na mustachi mnene, mwingine kidevu na mashavu yake yakiwa yame..
“Vipi, kaka kuna tatizo?” Mwanamke aliuliza. Alikuwa amevalia suruali ya jeans na tisheti nyeupe ya bia ya Serengeti. Mkono wake wa kuume alikuwa ameshikilia sahani ndefu ya plastiki iliyobebelea kinywaji cha Balimi.
“Hamna tatizo dada,” Jona alijibu akipangusa uso. Alinyanyua kinywaji chake akapiga mafundo mawili. Mwanamke alimtazama kwa mashaka. Ni wazi alikuwa anastaajabu kutingwa kule kwa mwanaume huyo.
.
“Samahani,” akasema. “Nilitaka kujua kama utahitaji chochote toka jikoni.”
“Ooh, kuna chakula gani?” Jona akauliza akiketi vema kitini.
“Nyama ya kukaanga, rosti, ndizi, chips na ugali.”

Jona akatazama saa yake ya mkononi. Muda ulikuwa umeenda, na pia alihisi uchovu. Aliona ni vema akabeba chakula moja kwa moja aende nacho nyumbani, hivyo akaagizia na kungoja.
.
Baada ya muda mfupi, chakula kikaletwa, akalipia na kuondoka.
Toka hapo bar mpaka nyumbani kwake si mbali. Mwendo wa wastani ungekufikisha kwa takribani dakika kumi. Kama ukikazana unaweza kuchukua hata dakika tano tu. Ila Jona hakuwa na haraka na nyumbani. Hakuwa na cha kuwahi, labda kama kungekuwa kuna mvua ingemkimbiza. .
.
Mvua ilikuwa imekata, manyunyu tu ndiyo yalikuwa yanashuka. Nyumbani hakukuwa na mtu wa kumngojea, anaishi peke yake. Miguu yake ilitembea taratibu akitazama chini. Alipokaribia nyumbani kwake, akaona kuna gari limesimama kwa mbele, shaka likampata.
Alisimama upesi, akalichambua gari hilo. Alisogea kidogo apate kuliona vema. Mara akagundua ni lile lile aliloliona kule kazini likiwa limesimama, na kisha kuondoka.
Lilikuwa ni Range Rover Sport, pleti namba yake ya Kenya.
Jona akajikuta anapata maswali. Akiwa hapo anaendelea kutazama, akamuona mwanamke mmoja akitokea gizani, akapanda ndani ya gari hilo upesi. Mavazi ya mwanamke huyo yalimfanya Jona aamini ndiye yule mwanamke aliyemtembelea kazini akidai mzigo wa Beatrice.
Ina mana amenifuata nyumbani? Alijiuliza. Kumbe ndiye yeye aliyekuwa ndani ya gari hilo kule nje ya mabanda!
.
Hakutoka hapo alipokuwa amejibanza. Macho yake yaliendelea kutazama gari akingojea liondoke. Aliminya mfuko wa chakula, akasonya.
.
.
“Chakula kinapoa.
.
Punde anamuona mwanaume mmoja mrefu akiwa kando na gari. Hakujua ametokea wapi. Mwanaume huyo aliegeza mikono yake dirishani mwa gari akasimama hapo kwa muda kidogo. Bila shaka alikuwa anaongea jambo na mtu ama watu waliomo ndani ya gari. .
.
Alitazama huku na kule, akapanda kwenye chombo wakaondoka. Jona alisindikiza hilo gari mpaka lilipoyoyoma kisha akatoka alipokuwa na kuenenda nyumbani kwake. .
.
Ilikuwa ni nyumba ya wastani, sebule na vyumba viwili, yenye uzio mfupi wa tofali na geti dogo jeusi. Ilikuwa kimya na tulivu sana, pia ilikuwa giza. .

Jona alikula kisha akaelekea chumbani kwake pasipo kupoteza muda. Kilikuwa ni chumba kipana kidogo, kitanda kikubwa na kabati moja kubwa la nguo lenye kioo kipana. Pembezoni mwa kabati hilo kulikuwa kuna kitu kikubwa chenye pembe nne kikiwa kimefunikwa na shuka la kijivu.
Jona alioga, kisha akafungua kabati lake na kitoa kisanduku fulani cha mbao, kidogo kwa umbo. Alikifungua, ndani yake kulikuwa kuna brashi kadhaa za kuchorea, mirija kadhaa ya rangi na penseli za mikaa, charcoal pencils.
.
Alikiweka kisanduku hicho juu ya stuli aliyosogeza karibu na kitu kilichofunikwa na shuka, kisha akalibandua shuka hilo. Kumbe hapo kulikuwa kuna makaratasi lukuki meupe marefu, mahususi kwa ajili ya kuchorea.
.
Karatasi ya kwanza kabisa ilikuwa ina picha ya mwanamke mrembo mwenye nywele za rasta. Jona aliitazama picha hiyo kwa sekunde kadhaa akifikiria jambo.
.
Mwanamke alikuwa anatabasamu, macho yake yaliangaza. Jona naye akajikuta anatabasamu, ila macho yake yakiwa mekundu.
.
Alifungua picha nyingine, picha ya mtoto wa kiume mwenye makadirio ya miaka mitatu.
.
Alitazama picha hiyo kwa sekunde kadhaa kabla hajaigeuza na kukutana na karatasi mpya isiyo na mchoro wowote. Hapo akaanza kuchora kwa kutumia penseli.
Hakutazamia popote pale isipokuwa alirejea kichwani mwake. Alichora picha ya mwanamke, yule aliyekuja kumtembelea ofisini akidai mzigo wa Beatrice. Alimchora mwanamke huyo hivyo hivyo kama anavyoonekana kuanzia kichwani mpaka kifuani asisahau hata vazi.
.
Alipomaliza aliketi kando, akitazama picha hiyo kwa umakini. Alijiuliza maswali kadhaa lakini hakuyapatia majibu. Alitamani Beatrice angekuwepo karibu ili amuulize, au basi angekuwa na simu ampigie.
Mwishowe anaamua kuipuuzia, anafuata jokofu sebuleni na kutoa chupa kubwa ya whisky anayoanza kuigida akielekea chumbani. Alikunywa chupa yote, kisha akalala.
.
Hawezi kulala pasipo kufanya hivi. Hujaza jokofu lake mara kwa mara kwa vileo vikali, kwa kazi moja tu, kumsaidia alale.
.
Asipokunywa, usingizi huwa mrefu kupitiliza. Ataamka na kushtuka kila mara. Hatapata amani.
Amekuwa akifanya hivi kwa takribani miaka mitatu sasa. Tangu pale alipoacha kazi yake ya uaskari, akiwa inspekta mwadilifu. .
.
.
Ni miaka hiyo ya nyuma, mwanaume Jona alifika kazini akiwa tayari amechoka. Amechoshwa na mawazo. Hakushika kazi yoyote akitafakari kwa dakika kadhaa. Alitoa kiti ndani akakiweka nje alipoketi kutazama mazingira.
Hii ndiyo ilikuwa desturi yake. Kila anapokumbana na jambo analohitaji kulifikiria vema, basi hutafuta mahala tofauti atakapopata hewa safi na kumtoa kwenye mazingira ya mazoea.
Bado mazingira yalikuwa ya giza, giza la asubuhi. Magari yalikuwa yanakatiza barabarani mara kwa mara watu wakienda makazini. Fremu za maduka zilikuwa zinafunguliwa, sauti za milango ya bati zikasikika huku na kule.
Lakini yote hayo hayakutosha kumuondoa Jona fikirani. Alijikuta anasonya kisha akachomoa simu mfukoni, ile aliyokabidhiwa na mwanamke aliyenadi kuagizwa na bwana Eliakimu Mtaja.
Akaifungua na kuzama mtandaoni. Akaperuzi vichwa vya habari vya magazeti apate kujua kinachoendelea nchini na duniani kwa ujumla.
Kwa muda mrefu sana hakufanya hilo zoezi. Alijiweka mbali na ulimwengu kabisa, si kwasababu ya kutokuwa na simu bali kwasababu ya kutotaka bughdha za ulimwengu. Aliuchoka, akataka mapumziko.
Ila kwa sasa, kwa namna mambo yalivyokuwa yanatukia, aliona kuna haja ya kupitia na kufahamu mambo kadhaa. Pengine anaweza pata jambo muhimu la kumpa mwongozo.
Alipitia vichwa vya magazeti nane. Miongoni mwao kichwa kimoja kikamgonga kichwa na kumpa hamu ya kutaka kujua zaidi. Kichwa hiki kilijirudia kwenye magazeti matano. Kilikuwa kinahusu mauaji ya mfanyabiashara ndani ya jiji la Dar es salaam.
“Mfanyabiashara auawa na majambazi.”
“Mfanyabiashara, almaarufu Bite wa China, auawa kwa risasi na watu wasiojulikana.”
“Majambazi wamvamia na kumuua Bite!”
Kusaka undani zaidi wa taarifa hiyo, Jona akazama tena mtandaoni. Akaperuzi blogu kadhaa zilizojaribu kuelezea tukio hilo, hatimaye akakata kiu yake ya habari.
Kwa msaada wa picha za mlengwa na taarifaze, aligundua kumbe aliyeuawa ni Beatrice Shauri! Hili likamshtua.
Si muda mrefu sana nyuma mwanamke huyo alionana na Jona akamkabidhi kazi ya kufanya aliyoahidi kumlipa pesa nzuri. Bado Jona alikuwa anamkumbuka vizuri mwanamke huyo kwa tabasamu na sauti tamu.
Alikumbuka hadi nguo alizokuja nazo siku hiyo alipoingia naye kwenye mahusiano ya kibiashara. Alikuwa amevalia suruali ya jinsi ya kubana na topu ya pinki. Nywele zake zilikuwa fupi, amezikata na kuzirepea vema.
Ameuawa!?
Jona aliacha shughuli zake akaufuata ule mzigo wa Beatrice Shauri, akautazama kwa kina. Ni kana kwamba kuna kitu alikuwa anatafuta. Japokuwa kazi hiyo aliifanya yeye mwenyewe kwa mikono yake, ila hakuwa amepata wasaa wa kuiperuzi.
Mzigo huo ulikuwa mkubwa. Picha kubwa ya kuchorwa kwa mkono ambayo kama ungeitazama vibaya, basi ungesema imechukuliwa na kamera, tena yenye uwezo wa hali ya juu.
Ilikuwa ni picha ya kisiwa kilichozingirwa na maji ya bahari. Kisiwa hicho kilikuwa cha kijani. Kilivutia machoni. Ukitazama vizuri pia hapo hapo pichani utaona ndege wekundu na weupe, upande wa kusini mwa kisiwa, wakiwa wanaruka pamoja.
Kulikuwa kuna vialama na viashiria vingi pichani. Jona alishindwa kuving’amua. Kwa mara ya kwanza, wakati anavichora, hakuvijali ila kwa sasa anapata mushkeli na kuumiza kichwa.
“Kwanini hii picha inatafutwa?” alijiuliza. Alitafakari kwa sekunde tano kabla hajaamua jambo kichwani:
“Ni lazima itakuwa na mahusiano na kifo cha Bite.”
Akaketi kitini akiendelea kutafakari na picha ipo mkononi. Akili yake ilimwambia kabisa wale watu aliowaona jana usiku nyumbani kwake watakuwa wanahusika na kifo cha Bite kwa namna moja ama nyingine.
Lakini je sababu itakuwa ni hii picha? akaitazama tena.
Maswali hayo yalikuwa magumu na majibu yake yalihitaji jitihada. Kama kuna siku mwanaume huyu alitamani kurudia kazi yake ya upelelezi basi ni hii. Alitamani kujua zaidi kuhusu Beatrice na ile picha.
Alikuja kuondolewa kwenye lindi hilo la mawazo na mlio mkali wa simu. Alikuwa ni Mh. Eliakimu Mtaja. Pasipo kufikiria mara mbili, Jona akapokea na kuitweka sikioni.
“Naongea na Johnathan Mchau?” Sauti kavu iliuliza.
“Ndiye mimi.”
“Kijana, naomba tukutane, nina shida nawe. Nimekutafuta kwa muda mrefu sana.”
Jona hakuona tabu, akakubali wakapanga miadi. Bwana Eliakimu alimsisitizia na kumwomba sana asije akakosa.
“Nakutegemea sana,” alisema kisha akakata simu.
Ilikuwa ni saa moja sasa ya asubuhi. Mwanga wa jua ulishatawala na kuangaza. Haikupita muda mrefu, akaja mwanaume mmoja mfupi rangi maji ya kunde. Macho yake makubwa, ndevu lukuki kwenye taya.
Mwanaume huyu anaitwa Jumanne. Ni mfanyakazi mshirika na Jona ndani ya banda moja. Ni maarufu sana kwa uchoraji, haswa michoro ya tingatinga.
“Afadhali umekuja,” Jona akasema baada ya salamu. “Kuna mahali nataka kwenda mara moja!”
Akaaga na kuondoka na mzigo wa Bite alioupitishia kwenye makazi yake. Baada ya nusu saa akawa ndani ya nyumba kubwa ya kuvutia. Mlinzi alimkaribisha na kumuelekeza mahali pa kukaa punde alipojitambulisha. Ilikuwa ni eneo dogo lililopo kwenye bustani, lina viti na paa dogo la kigae.
Muda si mrefu akatoka mwanaume mnene, mfupi, mweusi mwenye panki. Alikuwa amevalia tisheti nyeupe iliyobinuliwa na kitambi chake kikubwa, bukta na viatu vyepesi.
Akatazama kushoto na kulia kabla hajaenda kukutana na Jona bustanini. Walisalimiana na kujuliana hali kisha wakaelekea kwenye kiini cha mkutano.
“Jona, nina shida kubwa, na nimeambiwa wewe ndiye unayeweza kun’saidia. Ni muda mrefu sasa nimeliripoti polisi, lakini naona hamna kitu. Kama bahati tu, afisa mmoja akanambia nikutafute japokuwa alikuwa hana namna yoyote ya kukupata. Alichokuwa anakijua kuhusu wewe ni makazi yako tu, napo hakuwa na uhakika sana.”
Eliakimu akaweka kituo. Jona alikuwa anamsikiliza kwa umakini mkubwa.
“Ila naamini yote yatakuwa historia sasa maana nimeshakupata,” Eliakimu akaendelea kunena.
“Ni takribani mwezi mmoja sasa tangu mke wangu apotee. Nimemtafuta maeneo yote ninayoyajua, sijampata. Kwao na kwa marafiki zake! Napata mashaka sana juu ya hili. Nahofia usalama na uzima wake.
Jona, naomba unisaidie kumpata mke wangu. Nipo radhi kwa gharama yoyote ile ilimradi tu apatikane. Hata kama ameuawa, basi nijue na nani amehusika.”
“Mzee,” Jona akaita. “Sidhani kama ninafaa kufanya hiyo kazi. Sipo tayari kwa sasa.”
Uzuri bwana Eliakimu alishataarifiwa mapema juu ya ukaidi wa Jona. Mwanaume huyu alikuwa mgumu na mwenye msimamo mkali. Ilikuwa inahitaji roho ya nanga kumbadili fikra na mwenendo.
“Jona, nimekuomba hili kama mume anayemhitaji mke wake, baba anayemtafuta mama wa watoto wake. Si kwamba nakupa kazi, la hasha! Tafadhali naomba unisaidie.
Nipo radhi kukusaidia kwa namna yoyote ile. Nina mtandao mpana, ninafahamiana na watu lukuki wakubwa. Bila shaka itaweza kukurahisishia kazi.”
Uso wa bwana Eliakimu ulikuwa umenyong’onyea. Usingeweza kuamini kama mtu huyu, waziri wa Habari na michezo, angewahi kuja kuomba kitu kwa mtu wa kawaida kiasi hiki.
Watu hawa walikuwa wamezoa kutoa amri na maagizo na kisha jambo hutendeka. Ila kwa leo ilikuwa kinyume, alikuwa anaomba, tena kwa unyenyekevu.
“Mheshimiwa,” Jona akaita. “Hili jambo si la kukurupukia kabisa, linanihitaji niwe mtulivu.
Ningeomba unipatie usiku huu nilitafakari, nitakupa majibu.”
Bwana Eliakimu hakupendezwa sana na hilo jibu. Aliona kama vile Jona ametumia njia ya kistaarabu kukataa ombi lake. Ila hakuwa na namna, alipiga konde, akaamini.
“Sawa,” akasema kishingo upande. Jona akanyanyuka na kumpatia mkono wa kwaheri, akahepa zake.
Baada ya robo saa akawa ameshafika kazini. Alimkuta Jumanne akiwa ameketi anabofya kioo cha simu yake kubwa isiyo na jina.
“Vipi, kila kitu kipo sawa?” aliuliza.
“Shwari tu,” Jumanne akajibu na kuongezea: “Kuna mgeni alikuja kukuulizia. Yani ile we umetoka tu, akaingia.”
“Nani?” akauliza Jona akiwa anaketi.
Kwa mujibu wa maelezo ya Jumanne, Jona alipata picha halisi. Mgeni huyo alikuwa ni yule dada aliyekuwa anataka mzigo wa Bite.
“Bonge la ndinga mwanangu alikuja nalo, nikasema yees leo si ndo’ leo!” alisema Jumanne akitabasamu meno yote nje.
“Ulivyomwambia sipo akasemaje?” Jona alipeleleza.
“Akaniuliza vipi nyumbani kwako, nikamjibu haupo home.”
Jona akawa kimya akitafakari. Tabasamu la Jumanne lilififia akiuliza:
“Vipi mzee, kuna usalama?”
Jona hakutaka kumpa mashaka Jumanne. Alilazimisha tabasamu usoni akapachika kiganja begani mwa mwenzake.
“Kila kitu kipo sawa, J. Huna haja ya kuhofia.”
“Haya bana, ila huyo manzi ni mkali! Nifanyiefanyie basi na mie mwenzako ning’aze.”
“Sina hata namba yake. Hatujuani.”
“We si ndo’ zako hizo. Wazungu wewe, hadi na wabongo wewe. Sijui mie hawanioni?”
Kidogo Jona akapumzisha akili yake alipokuwa ananena na Jumanne. Walitabasamu na kucheka. Na siku ilikuwa hivyo mpaka jioni walipofunga wakiwa wameingiza USD 900 toka kwa watalii fulani wa kiamerika.
Kama kawaida Jona akapitia bar aliipoketi kwa masaa mawili akinywa Alvaro baridi. Hapa ni mahala pake mahususi pa kupunguzia muda wa kwenda kuwa mpweke nyumbani.
Alipomaliza akajikusanya na kuelekea nyumbani akitembea ado ado. Kichwani alikuwa na fikra mbalimbali zilizokuwa zinakatiza kwa awamu.
Alifika nyumbani, akashika geti. Ajabu likafunguka pasipo ku…  Huo ni utangulizi tu.. hii ni moja ya Riwaya refu sana +255 758 018 597


Post a Comment

0 Comments