“Mama
yangu na baba yangu naweheshimu sana lakini kwa kitendo hiki cha Mishel
kuondoka kimya kimya bila hata kuoga na kutoa sababu za kufanya hivyo ni kukosa
heshima kwa mume. Kama kulikuwa na tuhuma ilimpasa kuniuliza ili
nimwelezee. Hapa nilipo nimesimamishwa kazi kwa sababu ya Boss.
“Umefukuzwa
kazi?, kisa nini?”alihoji mama mkwe kwa mshangao.
“Nasingiziwa
tu vitu vya ajabu ambavyo sijavifanya. Na kilichotokea ni kwamba kuna
mwanamke alikuja na huyo mwanamke mpo ofisi moja sasa na uhusiano na boss na
uhusino huo umemfanya hasifanye kazi na mimi kuwa nafanya kazi sana. Mimi
kuhoji kwa nini ananiachia kazi zote ndo shida ilipoanzia. ”
“Pole
sana baba ingawa maelezo yako na ya mwenzio yanatofautiana. Sisi hatutaki
kumtafuta mkorofi cha msingi mtafute mke wako kisha mje tuyazungumze.
Nikushauri pia mwanangu ndoa yenu bado changa sana na mmetoka mbali sana jaribu
kukumbuka na usikubali kumpoteza mke wako kiurahisi. Usikubali kuachana
na mkeo maana umewekeza sana kwake. Umemsomesha mpaka amepata kazi.
Lakini usitumie wema huo kumnyanyasa. Yeye tulishaongea naye na
tutaendelea kumsahauri. ”Aliongea Baba mkwe.
“Nimewaelewa
wazazi wangu naomba mnisaidie kumpigia simu na kumweleza kuwa alichokifanya sio
kitendo cha uungwana kabisa. ”
“Sawa
baba tunashukuru kwa ujio wako pia tumegundua mengi. . Tutafikisha ujumbe wako.
Lucas
Manyama aliaga na kuondoka zake. Tofauati na siku zingine ambazo huwa
anamwachia pesa ya matumizi siku hiyo alikaa kimya hakutoa hata elfu 1.
Hiyo ilikuwa ni ishara kuwa amechacha na hana pesa. Aliamua kuondoka na
kurudi zake Musoma. Akiwa njiani aliendelea kutafakari juu ya mahali
ambapo mke wake angekuwepo. Kwa kuwa muda ulikuwa umeenda sana ilimlazimu
kwenda kulala Mwanza ili kesho ndo aende Musoma. Alivyofika Mwanza
aliamau kumtafuta rafiki yake kwa jina Kimaro. Huyu alikuwa ni rafiki
yake wa kufa na kuzikana tangia wakiwa chuo. Walipendana sana na waliishi
kama ndugu. Kimaro alipokea simu lakini ilionekana kama kulikuwa na
tatizo kidogo alionekana kuwa sehemu yenye kelele nyingi.
Kimaro
alimwandikia sms na kumueleza kuwa yupo sehemu moja hivi wanakula bata.
Lucas akamweleza kuwa na yeye yupo Mwanza stend. Kwa kuwa sehemu yenyewe
haikuwa mbali sana alimwelekeza afike hapo. Manyama hakutaka
kubisha na alienda moja kwa moja mpaka sehemu hiyo ambapo music wa bendi
ulikuwa ukipigwa. Aliingia huku akiwa na hofu kwa sababu mfuko wake
haukuwa vizuri. Watu walikuwa ni wengi sana na wenye furaha.
Alipewa kiti wakaketi na alimkuta rafikiye Kimaro akiwa tayari
ameshapendeza. Aliongea lugha za kuashiria alianza kulewa. Hakuwa
peke yake bali na mwanamke pembeni yake ambapo Lucas hakumtambua.
Lucas kwa haraka haraka alijua kuwa huo ulikuwa ni mchepuko wake tu. Na
yeye alikwa akinywa bia tena zile za bei ghali.
Lucas
alivyoambiwa aagize aliagiza maji jambo ambalo lilimfanya Kimaro kuwa mkali na
kusema apewe kinywaji anachotumia kwa sababu pesa sio tatizo. Baada ya
kulazimishwa aliamua kunywa ili kupunguza mawazo. Alikunywa pombe kali
kabisa na stori ziliendelea. Lucas alimweleza rafiki yake jinsi
anavyoumia kwa sababu mke wake ameondoka katika mazingira tatanishi.
Alimweleza kuwa hapo ametoka ukweni nab ado mke wake hayupo. Anaumia sana
maana hajui mkewe mahali yupo.
“Huna
haja ya kuumia toa taarifa polisi tu kuwa amepotea. Ahhhhhh kwa dunia ya sasa
mtu hawezi kupotea atakuwa yupo mahali amewekwa. Wanawake si viumbe
vya kuwaamini zaidi ni kuwaogopa sana maana wanaweza kufanya kitu kibaya na
ukajuta kumfahamu”.
“Ebu
tuyaache hayo maana yanaumiza naamini wapo wasichana wenye roho nzuri kama huyo
uliyekaa naye.
“Bora
hata umeliona hilo maana nilianza kuboreka” alisema mrembo huyo.
Waliendelea
kunywa na kula na sasa Lucas alianza kulewa. Watu kwenye ukumbi huo
walikuwa na raha na wengi walionekana ni watu wenye uwezo kifedha. Watu
na vitambi vyao walikuwa wakicheza mziki na kuomba nyimbo walizokuwa
wakizipenda. Ilikuwa ni burudani iliyoleta raha kwa kila ambaye alikuwa
eneo hilo.
“Eeeeeeeh!!!!!!!
yule si shemeji… yule au naona kwa makengeza ebu angalia”,Kimaro alisema huku
akionesha mkono kule mbele.
Lucas
ilibidi aangalie kule mbele. Hakuamini macho yake alipomuona boss
wake akiwa anacheza mziki na mkewe. Macho yalimtoka kama mjusi aliyebanwa
na mlango. Alianza kupiga hatua kuelekea mbele lakini rafiki yake
alimshika mkono na kumwambia.
“Haikupasi
kuwa na papara kwenye mambo haya. Tulia tuone mwisho wa mchezo huo”
“No
no I say no I cant tolerant any more(hapana, hapana nasema hapana siwezi
vumilia tena). . ” Lucas alinyanyuka kwa nguvu na kuanza kuelekea kule mbele
ambapo boss na mkewe walikuwa wanacheza.
Kimaro ambaye na yeye alionekana kuwa tayari ameshalewa alinyanyuka kwa nguvu na kumshika Lucas. Alitumia nguvu zake zilizochagizwa na pombe kumzuia na kumsogeza kwa pembenni.
Kimaro ambaye na yeye alionekana kuwa tayari ameshalewa alinyanyuka kwa nguvu na kumshika Lucas. Alitumia nguvu zake zilizochagizwa na pombe kumzuia na kumsogeza kwa pembenni.
“Ndugu
yangu nakuomba unisikilize kwa umakini sana kwa sababu ulimwengu huu sio wa
kutumia nguvu bali akili. Huyo ni mke wako sawa najua anauma kuliko kitu
kingine chochote ila sasa yupo na boss wako na wewe umesimamishwa kazi
tu. Kitu cha kujua ni kwamba hujafukuzwa kazi bali umesimamishwa kazi hivyo
lazima uwe mjanja ili kurudishwa kazini ikibidi huyo boss yeye ndo afukuze. .
“Nifanyaje
sasa”, Lucas alihoji kwa kuvuta pumzi. . Hasira zilimshuka kidogo.
“Unatakiwa
kutumia akili . Kwa kuwa Boss wako yupo na mkeo hapa tupate ushahidi wa
picha. Tukishapata ushahidi huo ni rahisi sana kuieleza jamiii kuwa boss
amekunyanyasa na anatoka na mkewe na pia anatumia fursa hiyo kukufukuza kazi.
”.
“Wazo
zuri sana sasa utawezaje kuwapiga picha bila wao kujijua na bila kuleta madhara
maana yule boss ni mkorofi sana”
“Hilo
niachie mimi wewe rudi kakae. Vaa roho ya ushujaa na uwe na amani kwa sababu
huu mchezo sisi ndo tutashinda.
Lucas
Manyama alionesha kuelewa na alirudi kukaa kwenye kiti na alishangaa kukuta
kuna msichana mwingine amekaa kwenye kiti chake. Macho hayana pazia kwa
sababu msichana huyo alikuwa akifanana kabisa na msichana wa mwanzo. Kwa
haraka haraka aliwaza na kugundua kuwa anaweza kuwa ni pacha wake.
Manyama alivuta kiti na kukaa. Alielekeza macho yake mbele na kuangalia kwa
makini kama kweli rafiki yake Kimaro anaweza kufanikisha kuwapiga picha.
Hakumwona hata huyo Kimaro jambo ambalo lilizidi kumchanganya.
“Shemeji
usiwe na wasiwasi wala usiwaze sana wanawake bado hawajaisha huku duniani na
kama kweli yule ndo mkeo na anayafanya yale huku wewe ukiangaika kumtafuta ili
kujua alipo basi huna chako. ”
Yalikuwa
ni maneno ambayo yalizidi kumuuma Lucas na kutamani kama angefanya kitu.
Bila kutarajia alinyanyuka na kusimama. Aliwaza kutoweka eneo hilo na
kwenda sehemu nyingine kabisa mbali na upeo wa vitu vya kuumiza vilivyokuwa
vikiendelea. Kimaro alimshika begani na kumwambia arudi kukaa.
“Vipi
umekamilisha huo mpango?”.
“Nimekamilisha
kwa kiwango kikumbwa”. Kimaro alijibu huku akimpa simu yake ili aweze
kuangalia. Aliziona picha na jinsi mkewe alivyokuwa amekumbatiwa na boss
wake. Alishindwa kujizuia machozi yalimtoka.
“Jamani
Lucas usiwe na roho ndogo hivyo wewe ni mwanaume usilie jipe moyo”alisema Yule
msichana aliyekuja mara ya pili. Msichana huyo aliongea kwa upole huku akitoa
kitambaa chake na kumpa afute machozi. Lucas alisista kukichukua lakini
mwanamke huyo kwa ujasiri alijisogeza zaidi na kumfuta machozi. Ilikuwa
ni faraja kwa Lucas kwani alichukua glass akaminiia kinywaji chake na
kunywa. Alikunywa kwa nguvu kisha kushusha chini. Aligonga meza kwa
nguvu kuwa aongezewe kinywaji. Muhudumu alikuja na kumuongezea.
Sasa ilikuwa ni kunywa kwa nguvu ili kutafuta stimu za kupunguza mawazo.
Kila mtu alikunywa kadri alivyoweza na nikama boss na mke wa Lucas walishtuka
na kutoweka ghafla eneo hilo. Wao wakabaki wanaendelea kula raha na
kujaribu usahau shida ambazo walikuwa nazo.
“Sasa
ni saa ya utambulisho, kila mtu akae kimya” aliropoka Kimaro.
Watu
wote walicheka maana kumbe wengine hapo mezani walikuwa hata
hawafahamiani. Kimaro akanza kujitambulisha yeye.
“Mimi
naitwa Godfrey Kimaro kijana mdogo mwenye mafanikio hapa mjini”. Wote kwa
pamoja walitabasamau.
“Mimi
naitwa Lucas Manyama mwanaume ambaye namiliki mke mzuri mjini lakni Boss
akanipokonya”. . Hapo kila mtu akaangua kicheko huku Lucas akitingisha kichwa
kuonesha masikitiko yake juu ya jambo hilo.
“Mimi
naitwa Julieth mpenzi wa kijana mwenye mafaniko hapa mjini”
“Mimi
naita Juliana pacha wa Julieth”.
“Safi
sana sasa timu imekamilika na hatuwezi kukubali mziki uishie chini. Kila
mtu amshike mtu wake tunaenda mbele kucheza. ” Kimaro aliongea huku akimnyanyua
Julieth. Pombe ilikuwa imekolea na hao taratibu walisogea mbele kwenda
kucheza mziki na kuwaacha Lucas na Juliana wakiwa wanaangaliana. Juliana hakuwa
na aibu maana na yeye pombe ilikuwa imekolea. Alisimama akajitingisha
tingisha kidogo kwa madaha nakuonesha ni jinsi gani alivyoumbwa
akaumbika. Macho kodoo macho ya Lucas yalimkodolea huku akimkagua kuanzia
kifuani kushuka chini. Juliana akanyanyua mkono mmoja kisha akampatia
ishara kuwa wanyanyuke. Lucas alikuwa ni mtu mwenye aibu sana hivyo
alikuwa akijifikiria kwenda mbele kucheza muziki. Lakini mikono laini ya Julaina
ilitosha kumsisimua na kumuinua kutoka pale kwenye kiti.
Hao
walisogea mbele na kuanza kucheza. Mbele kulikuwa na watu wengi hivyo
ilikuwa ni swala la kubambia kwa kwenda mbele. Sasa ilikuwa ni fursa ya
Lucas kuona ulimbwende wa binti huyo. Kwa kweli alichanganyikiwa na
alitamani hata kumtongoza usiku huo huo. Alijizuia lakini kitendoa cha
Juliana kuzungusha nyonga na kumtingishia makalio kilimfanya kumtamani
mlimbwende huyo. Juliana naye alimwonea sana huruma na aliamua kumfanyia vitu
ambavyo vingempa faraja usiku huo. Alikuwa akicheza na binti huyo huku
mawazo yake yakiwa kwa mtu aliyejitambulisha kuwa anaitwa Mama Vanesaa.
Aliifikiria ile sauti ambayo ilionekana ya binti mdogo kabisa na jinsi mwanamke
huyo alivyoamua kujitambulisha kwa jina mama Vanesa. Baadaye walirudi
kukaa na sasa walikuwa wameagiza nyama choma. Walikula na wakati
wakiendelea kula simu ya Lucas iliita na kuangalia alikuwa ni mama
Vanesa. Alikata na kumuomba amtumie sms kwa kuwa yupo kwenye kelele.
“Nimepata
dharura ambayo itanifanya kesho kutwa nisafiri hivyo nilikuwa naomba kama
hutojali tukutane kesho nikueleze matataizo yangu kisha tupange mikakati ya
kusaidiana kwa sababu matatizo yako tayari nayajua. ” Meseji kutoka kwa mama
Vanesa ilisomeka hivyo.
“Kula
brother nataka nikupe huyu mtoto Juliana ukalale naye upunguze hata mawazo.
”Iliingia meseji ingine kutoka kwa Kimaro.
Alitabasamau
kimoyomoyo na kujisemea kama litataokea hilo basi itakuwa bahati ya
mkenge. “Mtoto mzuri hivyo nitamla mpaka aimbe zeze”aliendelea kuwaza
huku akiweka finyango ya nyama mdomoni. Mara Juliana na yeye alichukua nyama na
kumlisha jambo lililozidi kumsisimua na kujikuta akitamani hata kumrukia muda
huo. Viungo vingine vya mwili navyo vilishasimama kwa hisia za mahaba…
Waliendelea na sasa Kimaro alikuwa akitumia jina lake na uwezo wake wa kushawishi kumtaka mpenzi wake Julieth aweze kumkubali Lucas na ikibidi ampe faraja usiku huo. Kwa hiyo kulikuwa na mawasilaino na watu walikuwa wakichati hapo. Julieth alikuwa akichati na Juliana na kumshawishi atumie uwezo wake wa kike kuwa na Lucas maana ni mwanaume mwenye mafanikio na huenda akawa mpenzi mzuri. Juliana hili swala kwake lilikuwa gumu kwa sababu tayari alikuwa na mpenzi mpya mara baada ya mchumba wake wa muda mrefu kuzinguana. Huyu mpenzi mpya alikuwa hafahamiki na mtu yeyote na ndio maana pacha wake alikuwa akimpigia chapuo ili kuona kama anaweza kuwa naye. Juliana hakuwa mjanja kama Julieth hivyo aliweza kumshawishi ingawa Juliana alikuwa akisingizia kuwa siku hiyo hakuwa poa labda siku ingine.
Waliendelea na sasa Kimaro alikuwa akitumia jina lake na uwezo wake wa kushawishi kumtaka mpenzi wake Julieth aweze kumkubali Lucas na ikibidi ampe faraja usiku huo. Kwa hiyo kulikuwa na mawasilaino na watu walikuwa wakichati hapo. Julieth alikuwa akichati na Juliana na kumshawishi atumie uwezo wake wa kike kuwa na Lucas maana ni mwanaume mwenye mafanikio na huenda akawa mpenzi mzuri. Juliana hili swala kwake lilikuwa gumu kwa sababu tayari alikuwa na mpenzi mpya mara baada ya mchumba wake wa muda mrefu kuzinguana. Huyu mpenzi mpya alikuwa hafahamiki na mtu yeyote na ndio maana pacha wake alikuwa akimpigia chapuo ili kuona kama anaweza kuwa naye. Juliana hakuwa mjanja kama Julieth hivyo aliweza kumshawishi ingawa Juliana alikuwa akisingizia kuwa siku hiyo hakuwa poa labda siku ingine.
Muda
ulizidi kwenda na baadaye Kimaro aliamua kutumia nguvu kwa maana alilipa vitu
vyote walivyokuwa wanadaiwa kisha waliiingia kwenye gari na safari ya kueleka
pasipojulikana ilianza. Kimaro alipakia gari kwenye moja ya lodge ambayo
ilikuwa inamilikiwa na baba yake. Julieth na yeye alishangaa maana
hakujua kama ilikuwa ni ya kwao. Walishuka na kuwa tayari alishaongea na
wahudumu wa hapo kuwa anakuja na wageni tayari alishawekewa. Alipewa funguo za
room zilizofuatana. Wakati Julieth na Julaina waliabaki wameduwaaa tu
wasijue nini kilikuwa kinaendelea. Julieth alikuwa akijiuliza maswali
mengi kwa nini siku hiyo huyo mwanaume hakutaka kumpeleka kwake kama alivyozoea
na kwa nini ameamua kuingia gharama hizo. Mwanzo alidhani kuwa walikuja
hapo kuwaleta Julaina na Lucas lakini aligundua sivyo mara baaada ya kuona
Kimaro akikabidhiwa funguo mbili. Kimaro yeye baada ya kupewa zile funguo
alimkabidhi moja Lucas na kumwambia kazi kwako. Alimshika Julieth mkono
na kuwaaga kwa kuwambia usiku mwema. Hao kwa mwendo wa madaha waliingia
kwenye chumba chao.
Juliana
na Lucas walibaki wamesimama na kuduwaha tu wasijue nini cha kufanya kwa wakati
huo. Waliangaliana na kila mmoja alionesha kuwa alikuwa akimwogopa
mwenzake. Waliogopana kwa sabbau mwaznoni hawakuwa na makubaliano ya aina
yoyote kuwa watalala pamoja. Lucas baada ya kuona mrembo yupo njia panda
na hana njia ingine ya kuondoka hapo alimkabidhi funguo. Juliana alisita
kuzipokea na kubaki amesimama akimshangaa tu. Lucas sasa iliamua kutumia
njia za kiume mara baada ya kugundua kuwa msichana huyo hawezi kuondoka.
Alimnyanyua juu juu na kwenda naye moja kwa moja mpaka kwenye chumba ambacho
walitakiwa kuingia. Hata Juliana alishangaaa mwanaume huyo amepata wapi
nguvu za kumbeba juuju. Alivyofika alifungua mlango kisha kuingia naye
ndani. Alimbwaga kitandani huku akihema kwa nguvu utadhani punda aliyeutua
mzigo mzito. Kweli wanaume wanakuwa na nguvu linapokuja swala la
mapenzi. Unaweza kukuta mwanaume ana kilo pungufu na mwanamke lakini akambeba
bila matatizo yoyote.
Juliana
alijilaza hapo kitandani huku akilaala na tumbo na kuacha kijungu mbinuo kikiwa
juu. Kinguo kifupi alichokuwa amevaa kilipanda kwa juu na kufanya weupe
wa majapa yake yaliyojazia kama godoro la Dodoma kuonekana. Lucas alipiga
magoti kisha kwa utaratibu alimvua viatu na kuvishusha chini. Juliana
alijigeuza na kupandisha miguuu juu ya kitanda kabisa.
“Ninaomba
uzime taa tulale”alisema mrembo huyo huku akipikichapikicha macho ishara kuwa
alikuwa akikerwa na mwanaga wa taaa.
Lucas
kabla hajazima taa alimshauri kitu. “Unaonaje kama ungeoga ili kupunguza
uchovu wa kukaa muda mrefu sehemu moja na joto la mwili ili uweze kulala
usingizi murua.
“Wazo
zuri lakini naona uvivu mwenzio ebu tulale kwanza alafu joto likizidi nitaoga”.
Juliana aliongea kisha kuvuta shuka na kujifunika. Lucas aliona ipo haja
ya yeye kwenda kuoga. Aliingia bafuni huku taswira ya umbo zuri la Juliana
likimtawala kichwani. Mawazo ya ngono yalikuwa yametawala akili yake kwa
kiwango kikumbwa sana. Alimaliza kuoga na kurudi zake chumbani.
Alifikiria cha kufanya kwa sababu ndo kwanza mwanamke huyo alikuwa amejifunua
shuka kuashiria kuwa taryari joto lilimzidia. Kitendo hicho sasa
kilifanya utamu wa binti huyo kuonekana. Lucas uzalendo ulizidi kumshinda
na kukuta viungo vyake vya siri vikimsisimka. Mkuki ulisimama wima tayari
kwa mapambano. Alipanda kitandani na kulala. Dakika mbili
hazikuisha alimsikia yule binti akinyanyuka na kuingia maliwatoni. Kabla
hajaingi aliwasha taa na kumfanya Lucas kuangalia kwa jicho la wizi binti huyo
alitaka kufanya nini. Kwa macho yake alimuona binti huyo akichojoa nguo
zake kisha kuingia bafuni… Tukutane whatsapp mtu wangu +255 758 018 597
Email - emanmic@yahoo.com
Email - emanmic@yahoo.com
0 Comments
Karibu sana, tuma ujumbe whatsapp +255 758 018 597 kujipatia simulizi zetu
Emoji